MH IDD AZZAN
MBUNGE wa
Kinondoni (CCM), Idd Azzan, amesema yupo tayari kujiuzulu ubunge, ikiwa
itabainika anajihusisha biashara ya dawa za kulevya. Kauli hiyo imekuja
siku chache baada ya kutajwa katika moja ya barua iliyosambazwa katika
mitandao ya kijamii, baada ya mtu anayedaiwa kukamatwa China na kuwatuhumu watu kadhaa akiwamo Idd Azzan.
Akizungumzia kuhusu sakata hilo jana, alisema hatua ya kuhusishwa na
biashara haramu ya dawa za kulevya, ni kutotenda haki mbele ya jamii
hasa wapiga kura wake na Taifa kwa ujumla.
Alisema mtu
aliyendika barua ya tuhuma dhidi yake, ni wazi amedhamiria kumshushia
heshima na huenda akawa ana jambo limejificha.
“Ni kweli
nimeiona hiyo barua katika mtandao, inayodaiwa imeandikwa na kijana
ambaye amekamatwa Hong Kong nchini China. Lakini ninajiuliza kama kweli
yeye ni raia mwema, katika hili kwanini hakutaka kutaja jina lake kwenye
barua hiyo.
“Hata nilipoisoma nimebaini kuwa huyo mtu
ametumika na huenda kabisa hayupo nje ya nchi, kwani katika maelezo yake
anataja jina la Balozi Philip Marmo kuwa amemsaidia hali ya kuwa hivi
karibuni Rais Kikwete alimteua Balozi mpya Abdulrahman Shimbo na Marmo
kuwa Balozi wa Shirikisho la Ujerumani.
“Kingine naona
alijaribu kuandika uongo kuweza kuaminisha jamii, kwani hata hilo jila
la balozi mwanzo limetajwa jina la Bernad na kukatwa kwa wino. Ninapenda
kulieleza Taifa kuwa naomba vyombo vya usalama vifanye uchunguzi wa
jambo hili na nikibainika ninauza dawa za kulevya nipo tayari kujiuzulu
ubunge wangu.
“Kubwa haki itendeke katika kufanya uchunguzi wa
jambo hili, ila ni lazima jamii na Watanzania kwa ujumla tusikubali kwa
makusudi watu waichafue nchi yetu kwa chuki na fitna tu,” alisema Azzan.
Alisema kutokana na hali hiyo, anashindwa kuchukua hatua yoyote ya
kufanya zaidi ya kuliandikia barua Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi
dhidi ya barua hiyo kuweza kubaini ukweli wa jambo hilo.
“Sijawahi kuuza dawa za kulevya na hata katika familia yangu hakuna mtu
anayefanya biashara hiyo haramu. Kila mmoja anajua kuwa Idd nilikuwa
Diwani wa Kata ya Magomeni, huku kazi yangu kubwa ikiwa ni biashara ya
magari na daladala ambayo ninaendelea nayo hadi sasa mbali ya ubunge
kama nilivyopewa heshima na wapiga kura wangu wa Kinondoni,” alisema
Azzan.
Alipoulizwa kuwa ni hatua gani ikibainika hakuna ukweli
wa jambo hilo baada ya vyombo vya usalama kufanya uchunguzi, alisema
atakachokifanya anamuachia Mungu.
“Ni ngumu kusema hatua gani
nitachukua ikibainika hakuna ukweli, lakini nataka kusema kama yule
aliyeandika barua hii angetaja jina lake ni wazi baada ya uchunguzi
ningeweza kuomba ushauri kwa mwanasheria wangu hatua za kuchukua, lakini
kwa kuwa hakutaja jina ni ngumu kuweza kuamua,” alisema Azzan.
Kwa mujibu wa taarifa zilitolewa kupitia mitandao, ziliripoti kukamatwa
kwa Watanzania wawili nchini China wakiwa na dawa za kulevya zenye
thamani ya Dola milioni 3.34 za Marekani.
BONDE FC NI MABINGWA WAPYA WA BEIRA YOUTH CUP 2012
-
Timu ya Bonde fc jana iliibuka kuwa mabingwa wapya wa BEIRA YOUTH CUP 2012
ubingwa huo umepatikana baada ya kuibuka na ushindi wa gili 5-4 dhidi ya
New Bo...
11 years ago
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA