Meya Kinondoni Awataka Watanzania Kufanya Mazoezi tiba.
MEYA wa
Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Songoro Mnonge ameiasa Jamii ya
Kitanzania kuwa na desturi ya kufanya mazoezi
tiba angalau mara moja kwa wiki kwa manufaa yako mwenyewe.
Songoro
aliyasema hayo alipoalikwa kuwa Mgeni rasmi wakati wa sherehe za maadhimisho ya
mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa Taasisi ya Mazoezi tiba ya Kisiwani Clinic
Centre(KCC) yenye makazi yake Mwananyamala Kinondoni jijini Dar es Salaam
ambayo sherehe zake za kutimiza mwaka mmoja zilifanyika mwishoni mwa wiki
Viwanja vya CCM ,Mwinjuma Mwananyamala Dar es Salaam.
Songoro
aliipongeza KCC kwa juhudi inazozifanya za kusaidia jamii kwani wanaisadia
Serikali kupunguza gharama za matibabu kwa wagonjwa wa magonjwa yasiyoambukizwa
na Serikali imeliona hili.
Aidha Meya
Songoro alimuomba Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni ambaye pia alihudhuria
sherehe hizo kuwa mwakani watenge bajeti ya shughuli zinazofanywa na jamii kwa
kujitolea kama hizi naye kama Meya atazisimamia kuhakikisha zinapitishwa kwa
maufaa ya jamii badala ya vikundi kuchangishana.
Songoro
alimaliza kwa kuwapongeza KCC kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kukusanya umati mkubwa wa kuhamasisha
jamii kufanya mazoezi tiba na kuimba jamii basi ihamasike kweli kwani kauli
mbiu ya maadhimisho haya kila mmoja inamhamasisha kweli afanye mazoezi kwani ni
dhahili “Afya yako mtaji wako” ni kauli mbiu nzuri bila afya bora huwezi kuwa
na manufaa kwa jambo lolote kwenye familia yako mpaka jamii inayokuzunguka.
Nae Mganga
Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni alitoa shukrani kwa taasisi ya kujitolea ya KCC
kwa kazi kubwa ya kukuzanya umati wa zaidi ya 2000 kuhamasisha jamii kufanya
mazoezi kwa kauli mbiu ya “Afya yako Mtaji wako”
Pili
aliahidi kushirikiana na KCC pamoja na vikundi vingine vya kusaidia jamii
vyenye mlen go kama KCC Daima katika zoezi dhima la kuisaidia jamii kuondokana
ama kupunguza magonjwa yasiyoambukiza.
Laiza
alimaliza kwa kuahidi kushirikiana na Taasisi kwa kuwakilisha bajeti za vikundi
kama KCC ili kupunguza maumivu ya vikundi kuchangishana ili kufanya hamasa ya
kusaidia jamii ifanye mazoezi kwani tutakuwa tunaisaidia Serikali kufunguza
Madawa ya kuhudumia Wagonjwa kadhaa wa magonjwa yasiyoambuza.
Nae mratibu
wa maadhimisho ya sherehe za mwaka mmoja wa KCC, Michael Machela alishukuru kwa shughuli zote kufanyika kwa
usalama na kwa kufana , ambapo maadhimisho yalihudhuliwa na vikundi vya Jogging
43 vyenye idadi ya Wanachama 25 mpaka 35 kila kikundi.
Lakini pia
kulikuwa na Wananchi ambao walifuata huduma za matibabu mbalimbali zilizoalikwa
katika maadhimishi hayo ambapo kulikuwa na JK Muhimbili ambao walikuwa wanatoa
huduma za Magonjwa ya Moyo, Ocean Road wenyewe walikuja na huduma ya Saratani
ya Mlango wa kizazi kwa kina Mama, Saratani ya Matiti kwa kina Mama na Saratani
ya Tezi Dumea kwakina Wanaume, KAM wenyewe walikuja na huduma ya Kinywa na
Manispa ya Kinondoni kupitia Hospitali ya Magomeni na Mwananyamala walikuja na
huduma ya Macho, Sukari, Shinikizo la damu, kupima uzito, kuchangia damu pamoja
na ushauri wa kitaalamu.
Kwa ujumla
maadhimisho ya Kisiwani Clinic Centre yalihudhuliwa na Watanzania zaidi ya 2500
kutoka kona zote za jiji la Dar es Salaam.