TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. KAULI YA KOVA NI YA KUMUHUJUMU RAIS.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
KAULI YA KOVA NI YA KUMUHUJUMU RAIS.
Kufuatia tamko la Kamanda wa Kanda Maalum wa Mkoa wa Dar es Salaam la
kutoa Onyo kwa Waislama na kusema kwamba wanamshikilia Sheikh Ponda kwa
tuhuma mbili. 1 . Kutokana na Tukio la Morogoro 2 . Kukiuka Masharti ya
Kifungo cha Nje alichohukumiwa mwanzoni mwa Mwaka huu.
CUF-Chama
cha Wananchi kinatafsiri tamko hili kama muendelezo wa kile
kinachoonekana kuwa ni hujuma dhidi ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Hatuoni sababu ya Kamanda Kova kutoa Onyo kwa Waislam kwa jambo ambalo
Waislam wameshatoa tamko kupitia Amiri wao Sheikh Mussa Kundecha na
kuiomba Serikali kuunda Huru ya Kuchunguza tukio hilo. Tangu litolewe
tamko hilo hakuna Muslam yoyote alifanya jaribio lolote la kutaka kulipa
kisasi kwa Polisi au kwa Mtendaji yoyote wa
Serikali. Sasa kuna haja
gani ya kutoa Onyo kwa jambo ambalo Waislam wamesha kubali maelekezo ya
Viongozi wao ? Pili kutangaza kumshikilia Ponda akiwa
Hospitali ambako anapata Matibabu kwa kisingizio au kwa tuhuma za Tukio
la Morogoro au kukiuka masharti ya kifungo cha Nje ni hoja zisizo na
mashiko.
Suala la Morogoro Makao Makuu ya Jeshi la Polisi imeunda Tume
ya kuchunguza tukio hilo, na tayari tume imeshaanza kazi ya kukusanya
Taarifa kwa Watu mbali mbali Mjini Morogoro. Sasa wewe Kamanda wa Kanda
Maalum unahusikaje kwenye jambo hilo la Morogoro ?
Au umepewa maagizo ya
kumkamata Ponda na Tume ilioundwa toka Makao Makuu ? Iwapo umepewa
Amri, je Tume hiyo imeshakabidhi ripoti yake kwa IGP Saidi Mwema na
imependekeza Ponda akamatwe kwa tukio hilo kwamba yeye ndi muhusika
alimpiga risasi Sheikh Ponda ? (Hapa nina maana amejipiga risasi
mwenyewe ? )
Hivi Kova ni Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu ? Suala
la kukiuka Masharti ya Kifungo cha Nje, hivi Kova unayafahamu hayo
masharti na umepata agizo lolote toka kwa Haakimu au Mahaka ilimuhukumu
Sheikh Ponda ,kwamba umkamate kwa kuwa amekiuka Mashari ?
Maswali yote
haya , yanakupa majibu na mtazamo sahihi kwamba Kova unafanyakazi ya
kumuhujumu Rais. CUF-Chama cha Wananchi kinaitafsiri kauli ya Kamanda
Kova kama imelenga kutoboa Jahazi lililobeba hasira za Waislam katika
suala hili la kupigwa risasi Sheikh Ponda.
Kauli hii inapaswa kulaaniwa
na wapenda Amani wote. CUF-Chama cha Wananchi kinamshauri Kamanda Kova
kwa sio lazima kujibu kila jambo unaloulizwa na Waandishi wa Habari, na
ikiwa lazima kujibu, basi uwe na mapimo ya kile unachojibu kwa maslahi
ya Nchi na usijibu tu kwa maslahi yako.
Mwisho kabisa CUF-Chama cha
Wananchi kinamtaka IGP Kutoa ufafanuzi juu ya kauli tata za Kamanda
Kova.
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA