Aug 16, 2013

YANGA WAAHIRISHA MKUTANO WA DHARURA

                         Lawrence Mwalusako katibu mkuu

Uongozi wa klabu ya Yanga umeahirisha mkutano wa dharura wa wanachama wote uliokuwa ufanyike siku ya jumapili tarehe 18.08.2013 katika viwanja vya sabasaba ukumbi wa PTA jijini Dar es salaam saa 3:30 asubuhi kujadailiana juu ya suala la Azam TV kurusha michezo yake.
 
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu kwa niaba ya makamu mwenyekiti wa Yanga, katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako amesema mkutano huo umeahirishwa kufuatia kuwepo kwa kikao kati ya Naibu Waziri wa habari, utamaduni, vijana na michezo mhe. Amos Makalla na viongozi wa kamati ya Ligi, TFF, Azam Media na viongozi wa klabu ya Yanga.
 
Ifuatayo ni taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari; 
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:
 
Ikumbukwe kuwa hivi karibuni , uongozi wa Yanga uliitisha mkutano Mkuu wa dharura uliokuwa  ufanyike  tarehe 18 Agost 2013 viwanja vya sabasaba kwenye ukumbi wa PTA Saa 3:30 Asubuhi kwa lengo la kujadiliana na suala la Azam Television kurusha mechi za Yanga. Mkutano huo kwa sasa umeahirishwa kutokana na sababu  ifuatayo:
 
Tarehe 14.8.2014 Naibu Waziri wa Habari, Utamadun,Vijanai  na Michezo Mheshimiwa Amosi Makala aliitisha kikao cha pamoja, kilichojumuisha pande zote husika wakimwemo  wasaidizi wake, shirikisho la mpira wa miguu Tanzania(TFF),Mtendaji mkuu wa bodi ya Ligi ya vodacom , uongozi wa Yanga sc na uongozi wa Azam Media.
 
Baada ya kikao hicho yafuatayo ni makubaliano yaliyofikiwa
 
(a)Klabu ya Yanga itapata fursa ya kushiriki na kupitia katika utengenezaji wa mkataba  wa udhamini wa haki za matangazo na televisheni  wa Azam Media ili kujiridhisha na vipengele vyote vya mikataba kwamba kwa namna yoyote haviathiri klabu ya Yanga kufuatia uhusiano uliopo wa Azam Media wanaotarajiwa kupewa haki hizo na Timu ya Mpira  Azam FC moja ya timu pinzani ya Yanga kwenye ligi ya Vodacom
 
(b)Kuwepo na utayari kwa uongozi wa Azam Media kukutana na uongozi wa Yanga kuzungumzia mahusiano ya kibiashara yatakayo nufaisha pande zote mbili.
 
Hivyo basi baada ya kuzingatia hayo uongozi unapenda kutoa taarifa kwa wanachama wake kuwa mkutano uliopangwa kufanyika tarehe 18 Agosti 2013, viwanja vya sabasaba kwenye ukumbi wa PTA Saa 3:30 asubuhi umeahirishwa hadi mtakapotangaziwa vinginevyo, lengo ni kutoa nafasi na fursa kwa uongozi kufanyia kazi hayo yaliyotajwa hapo juu
 
Pia uongozi unawashukuru wanachama na wapenzi wote wa Yanga kwa kuonyesha ukomavu na kusimamia maendeleo  ya klabu yetu kwa Hali na mali, na uongozi Utaendelea kusimama IMARA katika kuijenga Yanga Mpya
 
Uongozi pia unawataka wapenzi wote kuja kwa wingi uwanjani kuishangilia timu yetu wakati wa mechi ya kugombea ngao ya hisani kuashiria ufunguzi wa michuano ya kutetea ubingwa tunaoushikiria  wa Ligi Kuu ya vodacom
 
Clement Sanga
Makamu Mwenyekiti
Young Africans Sports Club
16.08.2013
Kwa niaba ya website ya yanga

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA