Sep 3, 2013

Mh Bimani: Kusini Unguja musikubali kutumiwa na CCM kupiga kura kumi bila ya kuwa na maslahi bora


Mh Bimani 
 
Wajumbe wa mkutano mkuu CUF wilaya ya kusini Unguja wametakiwa kujitaarisha vyema kwa kugombe nafasi mbali mbali za uwongozi ndani ya chama hicho katika uchaguzi utakaofanyika mwezi wa kumi mwana huu.

Kauli hio imetolewa na mkurugenzi wa haki za Binadamu habari uenezi na mawasiliano ya umma wa chama cha wananchi CUF Mh,Salim Bimani wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano mkuu wa wilaya ya kusini Unguja uliokuwa na lengo la kujadili mambo mbali mbali katika harakati za kuendeleza chama hicho katika mkoa wa kusini Unguja.

Mkutano huo umeshirikisha wajumbe hamsini kutoka majimbo mawili ya wilaya hio ambayo ni Muyuni na Makunduchi na umefanyika Makunduchi.

Mh,Bimani wakati akifungua mkutano huo amesema kuwa chama cha wananchi CUF ndio chama pekee katika nchi hii ambacho kila lengo na dhamira ya kuhakikisha kinaivuusha Zanzibar na hatimae kuwa nchi yenye mamlaka kamili na kisha kutambulika kitaifa na kimataifa.

Amewataka wajumbe hao kuhakikisha wananfanya utafiti wa kina kabla ya chaguzi za chama zinazokuja hivi karibu ili kuepuka kuingiziwa virusi ndani ya chama jambo ambalo litaweza kutupotezea dhamira ya kuipata Zanzibar yenye uhuru wake kamili.

‘’Kama munavojua ndugu wanachama nchi yetu kwa sasa imekabiliwa na mambo muhimu sana miongoni mwa mwambo hayo ni hili la kuipata Zanzibar yetu hivyo basi hatuna budi kuungana na kushikamana vizuri juu ya hili na tusikubali katu mwengine kutuharibia’’alisema Bimani.

Aidha aliwafahamisha wajumbe hao kuwa chama cha wananchi CUF tokea zamani kilisimama na hoja ya serikali tatu kwa ajili ya maslahi ya wazanzibar waliowengine na sio serikali mbili kama ilivo hivi sasa ambavyo wenzetu wasioitakia mema Zanzibar kwa ajili ya maslahi yao binafsi wanavotaka,hiyvo kutokana na haya kuna kila haja ya wazanzibar wote kuzidi kukiunga mkono chama hicho kwa ajili ya maslahi ya nchi yao.

Wakati akiendelea kuzungumza na wajumbe hao aliwaasa kutokuchokozeka hususani katika kipindi hichi kizito kwa nchi yetu badala yake wawachie tu CCM na wazimu wao’’umeona wapi chama cha siasa takribani miaka hamsini sasa kinaongoza nchi bila ya kuwa hata na maendeleo kilichobaki kwao nikutukana tu majukwani kama sikuishiwa kisera unadhani ni nini pumbavu likipumbaa pumbaa nao ’’alieleza Bwana Bimani.

Alieza kwamba CUF ni chama kinachojua siasa hivo basi kutokana na taratibu za kisiasa CUF Hawezi kukaa hadharani na kujibu matusi kama wananvofanya CCM kwani huo ni ujinga wa hali ya mwisho na ni wazi kuwa kufanya hivo ni kuishiwa sera na ndio mwisho wa kifo chao.

Lakini pia aliwanasihi wajumbe wa mkutano huo kutokuwa waoga kabisa na wafanye jitihada za kuwashawishi vijana kugombe nafasi ndani ya chama hicho kwani vijana ndio tegemeo kubwa katika mustakbali wa nchi hii.

Hakuna asiejua kuwa CCM huwatumia vijana wa kusini katika kipindi cha uchaguzi ili wapige kura zaidi ya kumi lakini nataka niwaambie kuwa kwa sasa majimbo mengine wameamka na hawataki tena wasiohusika kupiga kura katika majimbo yao hivyo vijana watakaokubali kutumiwa na kujaribu tu kupiga kura sehemu zisizokuwa zao basi kitakachowafika shauri yao.

‘’Ni mara ngapi vijana wenu wametumiwa kupiga kura zaidi ya moja na je nyinyi mumefaidhika na maendeleo gani huku Makunduchi hadi leo hii,musikubali washawishini vijana waamke huu sio muda tena wakukubali kutumiwa na CCM wenye lengo la kuiweka nchi rehani eti kwa kwakuwa wanapewa alfu kumi baada ya kupiga kura’’alisema Bwana Bimani.

Hata hivyo aliowaomba wajumbe hao kutochoka kabisa na suala hili badala yake wasimame kidete mpaka pale watakapohakikisha Zanzibar inashika mamlaka yake na hatimae kupachika bendera yake umoja wa matafa.

Nae katibu wa CUF wilaya ya kusini Unguja Bwana Mohammed Kombo alimshukuru Bwana Bimani kwa kukubali kwake wito wa kuja kufungua mkutano mkuu huo wa wilaya ya kusini Unguja kukubali kwake nikuonesha mshikamo imara uliopo ndani ya chama hicho.

Lakini pia alimuhakikishia kuwa wao kama viongozi wa wilaya hio watafanya kazi kwa jitihada zote ili kuhakikisha kuwa wananchi wa kusini Unguja wanazidi kuamka na kuitakia mema nchi hii.

Mkutano huu mkuu wa wilaya ni mikutano ya kawaida ndani ya chama ambayo hufanyika katika wilaya zote za Unguja na Pemba kwa lengo la kuimarisha chama