May 22, 2013

KAGAME CUP DRAW & FIXTURE



Droo ya makundi kwa ajli ya mashindano ya Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati al-maarufu kama (KAGAME CUP) imefanyika leo mchana mjini Khartoum nchini Sudan huku Mabingwa watetezi wa kombe hilo timu ya Young Africans wakipangwa kundi C kwenye michuano hiyo itakayoanza 18 Juni - 2 Julai 2013.

Taarifa iliyotolewa na katibu mkuu wa CECAFA Nicholaus Musonye imeonyesha mashindano ya mwaka huu itakua na jumla ya timu 13 kutoka katika nchi 10 wanachama ambapo droo hiyo imegawanyika katika makundi 3 ya A,B,C.

Timu zitakazo shiriki mashindano hayo na nchi zinazotokea kwenye mabano ni : Al-Hillal, El-Merreikh na Al Shandy (Sudan), Al Nasri (Sudan Kusini), Yanga & Simba (Tanzania), Express (Uganda), Tusker (Kenya), APR (Rwanda), Vitaloo (Burundi),  Ports (Djbouti), Elman (Somalia) na Falcon (Zanzibar)

Aidha mashindano ya mwaka huu yameongeza zawadi kwa washindi kutoka kitita cha dola za kimarekani 60,000 mpaka kufikia dolla 80,000 ikiwa kuna ongezeko la dola 20,000 ambapo zawadi kwa washindi zitapangwa na kamati ya utendaji kabla ya mashindano kuanza. 

Mashindano ya CECAFA mwaka huu yatafanyika nchini Sudan katika miji ya El-Fashir na Kadugli ambayo ni miji iliyopo kusini mwa nchi ya Sudan yenye wakazi wapatao milioni 34 na eneo la ukubwa wa kilomita za mraba 1,886,068.
Makundi ya michuano hiyo itakayoanza mwezi ujao ni kama ifuatavyo:

KUNDI A: El-Merrekh -(Sudan), APR (Rwanda), Simba SC (Tanzania), Elman (Somalia) - EL FASHER

KUNDI B: Al-Hillal (Sudan), Tusker (Kenya), Al Nasri (Sudan Kusini), Falcon (Zanzibar),  Al Shandy (Sudan) - KADUGLI

KUNDI C: Yanga SC (Tanzania), Express (Uganda), Ports (Djibout), Vitaloo (Burundi) - EL FASHIR


 KAGAME CUP FIXTURE 18th JUNE - 2nd JULY 2013 (EL-FASHIR & KADUGLI - SUDAN)

DATETEAMTEAMGROUP/TIMEVENUE
18.06.2013.TUSKER SUPER FALCON B - 2:00 PMKADUGLI
 AL HILLAL AL NASRI B - 4:00 PMKADUGLI
19.06.2013.VITALOOPORTS  C - 4:00 PMEL-FASHER
20.06.2013.YANGA SC EXPRESS C - 2:00 PMEL-FASHER
20.06.2013.ELMAN FC APR FC A - 4:00 PMEL-FASHER
20.06.2013.SUPER FALCON AL NASRI B -2:00 PMKADUGLI
20.06.2013.TUSKER AL-SHANDY B - 4:00 PMKADUGLI
21.06.2013.EL MERREIKH SIMBA SC A - 4:00 PMKADUGLI
22.06.2013.EXPRESS FC VITALOO C - 2:00 PMEL-FASHER
 PORTS YANGA SC C - 4:00 PMEL FASHER
22.06.2013.AL NASRITUSKER B - 2:00 PMKADUGLI
 AL SHANDY AL HILAL B - 4:00 PMKADUGLI
23.06.2013APR SIMBA SC A - 2:00 PMEL-FASHER
 EL MERREIKH  ELAM FC A - 4:00 PMEL-FASHER
24.06.2013AL NASRI AL SHANDY B - 2:00 PMKADUGLI
 SUPER FALCON AL HILLAL B - 4:00 PMKADUGLI
24.06.2013. PORTSEXPRESS FC C - 4:00 PMEL-FASHER
25.06.2013.VITALOO YANGA SC C - 4:00 PMEL-FASHER
26.06.2013.AL SHANDY SUPER FALCON B - 2:00 PMKADUGLI
 AL HILLAL TUSKER B - 4:00 PMKADUGLI
26.06.2012.SIMBA SC ELMAN FC A - 2:00 PMEL-FASHER
 APR FC EL MERREIK A - 4:00 PMEL-FASHER
27.06.2013.REST DAYREST DAYREST DAY  REST DAY
28.06.2013.(23) B2 VS C2(24) B1 VS BEST QTBDKADUGLI
28.06.2013.(25) C1 VS A2(26) A1 VS B3TBDEL-FASHER
30.06.2013.WNR 23 VS WNR 25WIN 24 VS WIN 26TBD 
01.07.2013.REST DAYREST DAYREST DAYREST DAY
02.07.2013.LOOSER LOOSER 283RD - TBDEL-FASHER
  WINNER 27 WINNER 28  FAINAL - TBDEL-FASHER

 HABARI KWA NIABA YA  http://www.youngafricans.co.tz