Kikosi cha Young Africans kilichoanza katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar
Baada ya kujiandaa kwa takribani wiki moja sasa kwa ajili ya mchezo
wa siku ya jumapili dhidi ya watani wa jadi Simba SC, mabingwa watetezi
timu ya Young Africans leo wanarejea jijini Dar es salaam wakitokea
kisiwani Pemba ambako walikuwa wameweka kambi ya maandalizi ya mchezo
huo.
Kikosi cha Young Africans ambacho kinashika nafasi ya nne katika
msimamo wa Ligi kikiwa na pointi 15, alama tatu nyuma ya vinara wa Ligi
Kuu ya Vodacom Simba SC kitashuka dimbani siku ya jumapili kwa lengo la
kusaka pointi tatu muhimu na kujiweka katika nafasi nzuri kwenye
msimamo.
Young Africans ambayo
inanolewa na kocha mholanzi Ernie Brandts imefanya mazoezi ya mwisho leo
asubuhi ikiwa ni maandalizi ya mwisho kwa ajili ya mchezo huo na hakuna
ripoti ya mchezaji mgonjwa hata mmoja kuelekea kwenye mtanange huo.
"Sisi
tumejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo huo, vijana wangu wapo safi
kiafya, kifikra na morali ni ya hali ya juu, hivyo tuna kila sababu ya
kuendeleza wimbi la ushindi ukizingatia uwezo wa kikosi chetu kwa ujumla
hivi sasa" alisema Brandts
Aidha Brandts alisema anatambua
michezo ya watani wa jadi duniani kote huwa ni migumu lakini kwa sasa
haoni sababu itakayowazuia kuibuka na ushindi katika mchezo huo japokuwa
Simba timu nzuri pia.
Ushindi kwetu siku ya jumapili ni muhimu,
ni muhimu kwa sababu tunapigania kutetea tena ubingwa wetu kwa awamu ya
pili mfululizo, kikubwa tunawaomba wapenzi, washabiki na wanachama waje
kwa wingi kuwashangilia vijana wao watakpokuwa wanapeperusha bendera ya
watoto wa jangwnai.
Tayari shirikisho la soka nchini TFF imeshatangaza viingiilio vya mchezo huo ambavyo ni:
VIP A tshs 30,000/=
VIP B ths 20,000/=
VIP C tshs 15,000/=
Orange tshs 10,000/=
Blue tshs 7,000/=
Green tshs 5,000/=
"MUNGU IBARIKI YANGA"
"DAIMA MBELE NYUMA MWIKO"
BONDE FC NI MABINGWA WAPYA WA BEIRA YOUTH CUP 2012
-
Timu ya Bonde fc jana iliibuka kuwa mabingwa wapya wa BEIRA YOUTH CUP 2012
ubingwa huo umepatikana baada ya kuibuka na ushindi wa gili 5-4 dhidi ya
New Bo...
11 years ago
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA