THE CIVIC UNITED FRONT - CUF CHAMA CHA WANANCHI,
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI;
Ijumaa, 06/12/2013 - Dar Es Salaam.
CUF - Chama Cha Wananchi kimesikitishwa na msiba mkubwa uliolikumba
taifa la Afrika ya Kusini baada ya mwasisi muhimu wa taifa hilo, rais
mwafrika wa kwanza, mzalendo na mpingaji mkubwa wa siasa za ubaguzi,
Mzee Nelson Mandela "Madiba" kuaga dunia jana alhamisi majira ya saa
2.50 usiku.
CUF kama chama
kinachoamini kuwa dhana ya siasa na mapambano ya kidemokrasia lazima
vijikite katika kupigania "HAKI SAWA KWA WOTE", tumeumizwa sana na msiba
huu kwani mzee NELSON MANDELA alipigania haki sawa kwa wananchi wa
Afrika ya kusini, na aliapa kupigania usawa wa binadamu katika nyanja
zote hadi atakapoiaga dunia.
Mzee Mandela alikuwa ni tunu ya
dunia, ni kiongozi aliyeweza kuionesha dunia kuwa "Viongozi wa Afrika
wanaweza kuibadili dunia kuwa kisiwa cha amani, maendeleo, maridhiano na
kutobaguana kwa misingi yoyote ile".
Mimi binafsi nimemfahamu
Mzee Mandela kuwa kiongozi wa mfano wa kuigwa aliyetoa maisha yake yote,
kukubali kukaa gerezani zaidi ya miongo miwili ilimradi tu aone HAKI
INATENDEKA NA UTU WA MWANADAMU UNAHESHIMIKA, jambo ambalo
alilifanikisha. Ni wanadamu wachache sana wameweza kujitoa kiasi hiki.
Kwa niaba ya viongozi wote na wanachama wa CUF Tanzania nzima, natoa
pole kwa familia ya Mzee Mandela, ndugu jamaa na marafiki, Rais wa sasa
wa Afrika ya Kusini na Wananchi wa Afrika ya Kusini, kwa msiba huu na
tunawaomba sote kwa pamoja tuyageuze matendo ya kweli ya Mzee wetu
Mandela kuwa dira thabiti ya kujenga mazingira ya KUJALI NA KUTEKELEZA
HAKI SAWA KWA KILA RAIA bila kujali rangi yake, kipato chake, utaifa
wake n.k.
Aidha, CUF itapeperusha bendera zake nusu mlingoti
kuanzia leo Ijumaa tarehe 06/12 hadi siku ya jumapili tarehe 08/12/2013
kwa ajili ya kuomboleza na kuenzi mchango wa Mzee Mandela hapa duniani.
"Mzee Mandela amelala kwa amani, lakini matendo yake makuu yamelinda utu wa wanadamu"
Apumzike kwa amani. Amina.
Imetolewa na;
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba,
Mwenyekiti wa Taifa,
BONDE FC NI MABINGWA WAPYA WA BEIRA YOUTH CUP 2012
-
Timu ya Bonde fc jana iliibuka kuwa mabingwa wapya wa BEIRA YOUTH CUP 2012
ubingwa huo umepatikana baada ya kuibuka na ushindi wa gili 5-4 dhidi ya
New Bo...
11 years ago
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA