Kingwendu amliza mtayarishaji wa filamu, achukua mkwanja wa kushuti filamu na kutokomea Msumbiji
Mchekeshaji maarufu Kingwendu anatuhumiwa kumtapeli mtayarishaji wa
filamu za kitanzania ‘Bongo Movies’ ambaye pia ni mshindi wa tuzo za
ZIFF, Bondi.
Akiongea kupitia kipindi cha Filamonata cha 100.5 Times Fm,
kinachoongozwa na Monalisa na mama yake 'Natasha', Bondi amesema kuwa
alimlipa pesa mchekeshaji huyo ili aweze kuigiza kwenye filamu yake na
kusaini mkataba, lakini alipotea na kuelekea Msumbiji huku simu yake
ikiwa haipatikani.
“Nilimpa fedha ya advance akachikichia moja kwa moja kumbe ana shows
zake anaenda kufanya huko Mozambique. Kwa hiyo imefika siku ya kufanya
filamu ambapo nilikuwa nashuti mimi, Kingwendu hayupo na siku sita
amezima simu haipatikani.” Amesema Bondi.
Lakini kukosekana kwa Kingwendu kulimpa shavu mchekeshaji mwenzake
Bambo, “Nikaamua nifanye option B, Option B niliyofanya nikamtafuta
Bambo nikaongea naye, nikaelewana naye vizuri na tukafanya kazi.”
Ameeleza producer Bondi.
Naye Kambarage wa kampuni ya usambazaji wa filamu ya Steps
Entertainment, amesema kwa kuwa Kingwendu amevunja mkataba na
kumuingizia Bondi gharama za ziada, kampuni ya Steps imepanga kuongea na
Kingwendu na endapo ataenda kinyume watamfungulia mashitaka ili iwe
fundisho kwa wasanii wenye tabia kama yake.
Filamonata inakuwa hewani kila Jumapili kuanzia saa 5 kamili asubuhi hadi saa 7 mchana kupitia 100.5 Times Fm.
Unaweza kusikiliza pia kupitia tovuti hii. http://www.timesfm.co.tz
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA