Dec 18, 2013

Kingwendu asimulia sakata la utapeli, 'nilimdanganya Bond mama anaumwa ili nikapige dili Msumbiji', ameyamaliza na amesaini kuwa chini ya Steps Entertainment

Kingwendu asimulia sakata la utapeli,

Kingwendu Ngwendulile, kama anavyojiita kiutani, amefunguka kiundani kuhusu tuhuma zilizotolewa na muongozaji wa filamu wa kampuni ya Steps Entertainment, Bond.

Akizungumza na Maryam Kitosi katika kipindi cha Hatua Tatu cha 100.5 Times Fm, Mchekeshaji huyo amesimulia ‘picha’ ilivyokuwa hadi kufikia hatua ya kudhaniwa kuwa amefanya utapeli, na kwamba yeye hakuwa na lengo la kutapeli.

“Kiukweli ni kwamba, niseme tu labda kuna tamaa flani imenichukua. Kwa sababu mimi niliingia mkataba na Mr. Bond kwamba bwana tutengeneze filamu. Akaniuliza una kazi? Nikamwabia wiki hii niko free kama kawaida, akasema okay tutaianza filamu yetu jumamosi tarehe 16. Baadae akanipigia simu akaniambia, mtani wangu Kingwendu hii filamu tutacheza tarehe 19 siku ya jumanne kwa sababu namalizia kupiga rangi ile nyumba.” Amesimulia Kingwendu.

“Hapo hapo ananipa taarifa hiyo hapo na ikaja bonge la deal kutoka Mozambique kutoka serikali ya FRELIMO, unaona bwana bonge la issue ya go and return. Hebu niambie hata wewe, kwamba filamu inachezwa siku ya Jumanne tarehe 19, mimi nahitajika kwenda kupiga kampeni Jumapili, halafu Jumatatu narudi Dar es Salaam. Si naiwahi hiyo filamu ya bwana Bond?”

Kwa kutompa presha mtayarishaji wa filamu hiyo, Kingwendu aliamua kutumia ulimi wake vizuri, lakini bahati mbaya hakujua yatakayojili huko Msumbiji.

“Bondi ningemwambia kwamba mimi naenda zangu Mozambique angemaindi, kwa sababu tayari ameshaandaa kila kitu. Kweli huku na huku jinsi ya kufanya, nikamdanganya Bond mimi naenda kwa mama kwa sababu mama anaumwa, na kweli mama alikuwa anaumwa lakini bahati nzuri nilimtumia fedha (kwenye ile advance aliyopewa ya laki mbili), nikampa mama laki moja.” Kingwendu ameelezea mkasa huo.

“Kwenda kule, kumbe ile tiketi mimi sikuiangalia, kumbe ilikuwa tiketi ya kwenda tu. Sio go and return! Sasa siku ya Jumatatu nikaangalia tiketi naona tiketi sio ya go and return. Nikawaambia waheshimiwa mbona hii tiketi sio go and return na mimi nina kazi ya watu huko? Wakaniambia usiwe na wasiwasi, akatumwa mtu kwenda kukata tiketi ya Jumatatu, akarudi anasema ndege imejaa ipo ndege ya Jumatano.”

Kingwendu ameeleza kuwa alipoona mambo hayaendi na anahitajika Jumanne Tanzania, akatafuta line ya simu ya Msumbiji akampigia Bond lakini hakupokea , na hata aliporudi akamtafuta akawa hapokei simu na hata alipomtafuta hakuweza kumpata kiurahisi.

Hata hivyo, Kingwendu amedai kuwa alimpata Bond na uongozi wa Steps Entertainment wakakaa wakayamaliza. Na habari njema ni kwamba walimsaini moja kwa moja kuwa msanii wa kampuni hiyo.
Kwa hiyo Kingwendu yuko chini ya Steps Entertainment

chanzo na http://www.timesfm.co.tz

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA