Mar 6, 2014

SAMIA SULUHU AMEPOTOKA! ( CUF )

 http://zanzibarkwetu.files.wordpress.com/2012/04/suluhu-hassan.jpg
THE CIVIC UNITED FRONT
(CUF- Chama Cha Wananchi)

Office of the Secretary General
Party Headquarters,
P.O. Box 3637 , Zanzibar, Tanzania

6/3/2014

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Chama Cha Wananchi CUF kimeshangazwa na kusikitishwa na kauli iliyotolewa na Waziri wa Nchi afisi ya Rais anaeshughulikia mambo ya Muungano Samia Suluhu Hassan, wakati alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari na kuripotiwa na gazeti la Serikali Daily News la March 5/2014.

Kauli hiyo ni kuamini kuwa katiba ya Zanzibar itafanyiwa marekebisho na moja analoliamini kuwa ni kero ni sheria ya Zanzibar kuruhusu ardhi ya Zanzibar kumilikiwa na Wazanzibari peke yao.

Waziri Samia Suluhu Hassan, aliwaeleza wandishi hao wa habari ya kuwa anamini kuwa katiba ya Zanzibar nayo itafanyiwa marekebisho makubwa na marekebisho hayo yatalenga kile ambacho yeye anakiona ni kero kwa Muungano ni sheria ya Zanzibar inayoruhusu na kulinda ardhi ya Zanzibar kutomilikiwa na watu ambao sio Wazanzibari.

Waziri Samia Suluhu Hasan kwa mtazamo wake yeye kuwa kero moja ya Muungano ni kutoruhusiwa kwaa Watanzania bara kuruhusiwa kumiliki ardhi chache na ndogo iliyopo Zanzibar.

Jambo ambalo tunaamini si kwa bahati mbaya au kama hajuwi kuwa ardhi haikuwamo katika mambo kumi na moja ya makubaliano ya mambo ya Muungano, kila nchi ina sheria tofauti ya umiliki na usimamizi wa ardhi.

Bali mtazamo huu ni usaliti wa wazi wa Mapindauzi ya mwaka 1964 ambao lengo lake kuu moja wapo ni kuigawa ardhi chache ya Zanzibar kwa wananchi wa Zamzinar ili ilete tija na maendeleo kwao na Taifa kwa ujumla.

Chama cha Wananchi CUF kinamini kuwa kuna kero nyingi za Muungano kama Waziri wa Mungano kuzizungumzia kero ambazo zimeufikisha Muungao huu pahala pabaya, na kuzua malalamiko mengi hasa kwa upande wa Zanzibar kwa kupoteza mamlaka yake na uwezo wake kinyume na makubaliano yaliyounda Muungano huo wa mwaka 1964 .

Leo hii tunashuhudia tena kauli za kuendeleza dhamira ya kuipotezea Zanzibar Utaifa wake kwa lengo la kujikweza, kujipatia umaarufu kuwafurahisha wachache wasioitakia mema Zanzibar.

Chama Cha Wananchi CUF kinaamini ndani ya Muungano huu wa miaka 50 kumekuwa na kasoro nyingi na kubwa hali iliyopelekea rais wa
Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kuchukua hatua ya kuunda tume ya kukusanya maoni.

Ambapo hivi sasa Bunge malum la katiba linakutana kwa ajili ya kutengeneza katiba mpya ambayo tayari rasimu ya pili ya marekebisho imeshatoka.

Alichokizungumza Samia Suluhu ni kuinadi ardhi ya Zanzibar na kuiweka mnadani, na ukiondoa udhibiti huo wa ardhi kwa Wazanzibari ambao upo kisheria ni kufungua soko kwa watu takriban milioni 50 wenye uwezo kuivamia ardhi isiyozidi 2500 sq.km ya ardhi ya Zanzibar kwa maslahi ya Watanzania Bara wenye ardhi zaidi ya 950.000 sq.km, hali hiyo inaonesha wazi lengo na dhamira ya kuimeza Zanzibar


HAKI SAWA KWA WOTE

Salim Abdalla Bimani
Mkurugenzi Haki/H/Uenezi/Masiliano ya Umma

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA