UKISTAAJABU YA MUSSA UTAONA YA FARAUNI AJABU AL AHLY HAWAJUI MECHI ITACHEZWA WAPI
Katika hali ya kushangaza wenyeji timu ya Al Ahly mpaka sasa
wameshindwa kuwadhibitishia viongozi wa Young Africans pamoja na Ubalozi
wa Tanzania nchini Misri juu ya Uwanja utakaotumika kwa ajili ya mchezo
wa marudiano Klabu Bingwa Barani Afrika siku ya jumapili.
Sheria za mashindano ya CAF zipo wazi na zinaelekeza timu mwenyeji
wanapaswa kuwajulisha wageni uwanja utakaotumika kwa mchezo takribani
siku 10 kabla ya mchezo, huku mpaka leo siku ya jumatano takribani siku
nne kabla ya mchezo wakishindwa kutabanaisha mchezo utakapofanyika.
Mapema
jana mchana Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini Misri Bw Idrisa Juma
alifika makao makuu ya Al Ahly kuweza kujua taratibu za mchezo huo
lakini hakufanikiwa kupata majibu kamili zaidi ya kuahidiwa kufikia leo
mchana kwamba watakua wameshapata majibu juu ya ni sehemu gani mchezo
utafanyika.
Afisa Habari wa Young Africans Bw Baraka Kizuguto leo
asubuhi aliambatana na maofisa Ubalozi mpaka makao makuu ya klabu ya Al
Ahly na kukutana na meneja Said Abdoulaziz na meneja usalama Morgan na
katika mazungumzo hayo walisema mpaka muda huo walikuwa hawajapata
maamuzi ya serikali juu ya uwanja utakaotumika kwa mchezo.
"Tumeomba
mchezo ufanyike kati ya Uwanja wa Cairo au mji wa Alexandria lakini
Serikali imekataa kutoa Viwanja yake pamoja na ulinzi katika mchezo wetu
kutokana na washabiki wetu kufanya vurugu kwenye mchezo wa Super Cup
dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia" alisema Said.
Katika kikao hicho
kilichofanyika kwa zaidi ya masaa mawili Uongozi wa Young Africans
uliomba mchezo wake ufanyike jijini Cairo kwani ndo sehemu waliyojiandaa
kwa mchezo kufuatia taarifa ya Al Ahly walipokuja Tanzania kwenye
mchezo wa awali.
Mara baada ya mazungumzo hayo waliahidi kuongea
na waziri mwenye dhamana ya michezo kuruhusu mchezo ufanyike jijini
Cairo na kwamba mchezo huo kama iliyoamuriwa tangu awali na mamlaka
husika ya ulinzi na usalama hautakua na washabiki wowote kwa uwanja
wowote utakaochezewa.
Akiongea na mtandano rasmi wa klabu ya Young
Africans Kizuguto amesema wamekaa kusubiria majibu ya Uwanja
utakaotumika kwa mchezo zaidi ya masaa 6 bila majibu huku viongozi hao
wa Al Ahly wakipigiwa simu na kutopokea.
"Tuliwaambia jiji la
Cairol lina Viwanja zaidi ya 10 vyote vyenye hadhi ya kimataifa sio
lazima tucheze Cairo International, wajaribu kuomba viwanja vingine
lakini walionekana kutokua tayari na zaidi kusisitiza watamuomba waziri
wa michezo aruhusu mchezo ufanyike Cairo bila washabiki" alisema
Kizuguto
Kutokana na mazingira hayo ya ucheleweshwaji kutangaza
sehemu utakaofanyika mchezo Ubalozi wa Tanzania nchini Misri kupitia
Balozi wake Bw Mohamed Hamza na maafisa wake na uongozi wa Young
Africans umeendelea kufanya maandalizi kwa njia zote kuhakikisha timu
inafika salama na kupata huduma zote muhimu ikiwa ni pamoja na malazi,
chakula, uwanja wa mazoezi na ulinzi kwa kipindi chote timu itakapokuwa
nchini Misri.
Msafara wa watu 30 unatarajiwa kuwasili kesho
alfajiri jijini Cairo kwa shirika la Ndege la Egypt Air na kupokelewa
Uwanja wa Ndege na Balozi Hamza, pamoja na maafisa Ubalozi kisha
kuelekea sehemu maalumu ambayo timu ndipo itakapokua imeweka kambi mpaka
siku ya mchezo.
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA