Jul 4, 2012

Wakenya Kuchezesha Ngorongoro Heroes Nyumbani

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Kenya kuchezesha mechi ya raundi ya pili kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 kati ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) na Nigeria.

Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili itakayofanyika Julai 29 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam atakuwa Moses Ojwang Osano.

Waamuzi wasaidizi watakuwa Peter Keireini na Elias Kuloba Wamalwa wakati mwamuzi wa mezani (fourth official) ni Thomas Onyango. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Charles Masembe kutoka Uganda.

Pia CAF imemteua Alfred Kishongole Rwiza wa Tanzania kuwa Kamishna wa mechi ya michuano hiyo kati ya Misri na Kenya itakayochezwa jijini Cairo kati ya Julai 27, 28 na 29 mwaka huu.

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA