Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka
Kenya kuchezesha mechi ya raundi ya pili kuwania tiketi ya kucheza
Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 kati ya
Tanzania (Ngorongoro Heroes) na Nigeria.
Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili
itakayofanyika Julai 29 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
atakuwa Moses Ojwang Osano.
Waamuzi wasaidizi watakuwa Peter Keireini na Elias Kuloba Wamalwa
wakati mwamuzi wa mezani (fourth official) ni Thomas Onyango. Kamishna
wa mechi hiyo atakuwa Charles Masembe kutoka Uganda.
Pia CAF imemteua Alfred Kishongole Rwiza wa Tanzania kuwa Kamishna wa
mechi ya michuano hiyo kati ya Misri na Kenya itakayochezwa jijini
Cairo kati ya Julai 27, 28 na 29 mwaka huu.
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA