Feb 19, 2013

AZAM YAIPELEKA YANGA BAGAMOYO


Kikosi cha wachezaji 26 wa timu ya Young Africans kinaingia kambini leo mchana katika Hoteli ya KIROMO iiliyopo pembeni kidogo mwa mji wa Bagamoyo tayari kwa maandalizi ya mchezo wa ligi Kuu ya Vodacom siku ya jumamosi dhidi ya timu ya Azam FC katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Baada ya kuichapa timu ya African Lyon kwa mabao 4-0 katika mchezo uliochezwa mwishoni mwa wiki, Young Africans itashuka dimbani kuhakikisha inaondoka na ponti zote 3 ambazo zitaifanya iendelee kuongoza msimamo wa ligi kuu ya Vodacom (VPL) na hatimaye kutwaa Ubingwa huo.

Kocha Mkuu wa Yanga mholanzi Ernest Brandts amesema kuwa kikosi chake kipo fit kuelekea mchezo huo wa jumamosi, na anaamini mchezo huo ndio utatoa taswira halisi za msimamo wa ligi kuu ya VPL kuelekea kutwaa Ubingwa.

Namshukuru mwenyezi mungu, kikosi changu kipo katika hali nzuri, wachezaji wote 26 nimekua nao pamoja wakifanya mazoezi kwa nguvu,  wachezaji wote wanaonyesha viwango vya hali ya juu, hali inayonipa fursa ya kupata nafasi ya kumtumia mchezaji yoyote katika mchezo huo 'alisema Brandts'

Young Africans inaongoza  msimamo wa VPL kwa kuwa na pointi 36 huku ikiwa imecheza michezo 16, imeshinda jumla ya michezo 11, imetoka sare michezo mitatu (3) na kupoteza michezo miwili (2) huku ikiwa imefunga jumla ya mabao 33 na kufungwa mabao 12 tu.
Nafasi ya pili inashikiliwa na timu ya Azam FC yenye pointi 33 ikiwa na mabao 27 ya kufunga na ikiwa imefungwa mabao 14 na kesho itashuka dimba la Chamanzi kucheza na timu ya JKT Ruvu katika muendelezo w amichezo ya Ligi Kuu ya Vodacom.

Katika mchezo huo wa jumamosi  Young Africans inahitaji ushindi ili kuendelea kuongoza msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom pia itakua ni kuendeleza ushindi dhidi ya timu hiyo ya waoka mikate wa Bakhresa kwani michezo miwili ya mwisho watoto wa Jangwani waliibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Habari njema kuelekea katika mchezo huo ni kuwa kikosi hakina mchezaji majeruhi hata mmoja hali inayopelekea  kuwa na maandalizi mazuri ya mchezo huo wa jumamosi dhidi ya timu ya Azam FC.
Chanzo na  http://www.youngafricans.co.tz

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA