HIKI NDICHO ALICHOSEMA JANUARY MAKAMBA BAADA YA MNYIKA KUWEKA NAMBA YAKE YA SIMU
John Mnyika
kaweka namba yangu ya simu ya mkononi ili watu wanipigie na kutukana.
Nadhani ni siasa isiyo ya kistaarabu. Hadi sasa nimepata messages zaidi
ya 600. Sio sahihi kabisa.
Wabunge WOTE tulishindwa kupitisha
maamuzi yenye maslahi kwa mtu wa kipato cha chini. Harakati za
mitandaoni haziondoi ukweli huo. Vilevile, kodi hii imepitishwa tarehe
29 Juni 2013. Kwa Mbunge ambaye alikuwa na wajibu wa kulipinga siku hiyo
na kulisemea kuanzia tarehe 30 Juni 2013 kuamka leo na kutapatapa
mitandaoni ni unafiki mkubwa na ni siasa za kuangalia upepo unapovuma na
ni unafiki mkubwa. Namheshimu Zitto Kabwe
kwasababu alitoa kauli immediately ya kusema anaona aibu kuwa sehemu ya
Bunge hili na kwamba wawakilishi wa wananchi wamewaangusha wananchi.
Mwenzake John Mnyika anajitoa fahamu na kufanya harakati kupitia press
releases.
Suluhisho hapa sio kulumbana wala kutupiana lawama.
Suluhisho ni kurudi Bungeni na kubadilisha pale tulipokosea. Sio
kutafuta umaarufu mitandaoni. Kunapotokea kosa, tunasahihisha haraka
then we move on. Siasa sio kwenye kila jambo.
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA