Aug 19, 2013

SABABU ZA KUPIGWA RISASI SHEIKH PONDA ZATAJWA

·        SERIKALI YAAMBIWA IJIANDAE KUTUMALIZA,LAKINI UKWELI TUTASEMA TU.
·        UPENDELEO KWA WAKRISTO WAANIKWA.

Na mwandishi wetu wa munirablog;
Waislamu wamefahamishwa sababu zilizopekea Sheikh Ponda Issa Ponda kupigwa risasi hivi karibuni.

Hayo yaliwekwa wazi na Sheikh Suleyman Daud alipokuwa anawasilisha mada ya KWA NINI SHEIKH PONDA KAPIGWA RISASI.

Ameyasema hayo leo jioni katika viwanja vya Mwembe Yanga wakati Waislamu walipofurika kwa ajili ya kusikiliza tamko la Waislamu juu ya kadhia hiyo.

"Sheikh Ponda hakuwahi kuchochea bali Sheikh Ponda alikuwa anawasilisha madai ya Waislamu kwa Serikali na kuwajulisha Waislamu juu ya dhulma wanazofanyiwa kutoka kwa watawala wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi,

Sheikh Suleyman alibainisha madai hayo kuwa ni pamoja na Serikali kufanya upendeleo wa makusudi kwa Wakristo kwa kuyapatia mabilioni ya shilingi makanisa yote nchini kwa kila mwaka chini ya Memorandum of Understanding (MOU) ambao ulisainiwa mwaka 1992 ambapo Edward Lowasa alisaini kwa niaba ya Serikali.

Leo wakristo wana Mashule makubwa makubwa,wana Hospitali kubwa kubwa ni kwa sababu ya mapesa hayo ambayo sisi Waislamu ni sehemu ya walipa kodi.

Mbali ya hayo Sheikh Ponda amekuwa anakumbusha madai ya mauaji yaliyofanywa na polisi katika msikiti wa Mwembe Chai mwaka 1998 na Serikali hii hii kukataa kuunda tume wala kuwafikisha mahakamani wauwaji huku ikiunda tume ya kuchunguza mauaji ya mbwa yaliyofanywa na raia wa kigeni baada ya mbwa huyo kupewa jina la Immagration.

Aliendelea kusema kwamba Sheikh Ponda amekuwa anadai haki ya mtoto Chuki Athman aliyepigwa risasi kwa madai kakutwa na nyaraka za uchochezi,huku akihoji kama hiyo ni hukumu sahihi kwa mwenye kukutwa na kitu kama hicho.mtoto huyo hadi leo amepooza mwili.

Mwaka 2001 Imamu akitoka katika Swala ya ijumaa kule Zanzibar alipigwa risasi mbele ya msikiti kwa madai kwamba yeye alikuwa ni mmoja wa waliohamasiha maandano ya chama cha siasa ambayo yalikuwa yafanyike siku inayofuata.

Aidha Sheikh Suleyman alisema Sheikh Ponda alikuwa anaikumbusha Serikali mara kwa mara juu ya madai ya Waislamu juu ya dhulma na ukandamizwaji unao fanywa na Serikali hii ambapo mwaka 1989 Halmashauri kuu ya Waislamu iliyafikisha madai hayo kwa Rais wa wakati huo (Mkapa) ambapo yeye alijibu kwamba yeye pia ni rais wa wala nguruwe lakini baada ya miaka kumi (kwa maana mwaka 2009) madai hayo hayo tukayachapa katika kitabu na kuyafikisha katika idara zote za serikali kuanzia ngazi ya rais hadi ngazi ya chini (Mkuu wa wilya Tanzania mzima) lakini hadi leo serikali inajifanya kiziwi na inapokumbushwa mkumbushaji anaitwa mchochezi.

Ponda alikuwa anawauliza iweje waislamu waliobambikiwa kesi ya kuchoma kanisa pale Mbagala wamewekwa ndani hadi leo na wamenyimwa dhamana lakini wakristo waliochoma msikiti kule Tunduma hawajakatwa na hata vyombo vya habari havikuripoti,haki na uadilifu uko wapi.

Mbali ya hayo kuna dhulma lukuki katika Sekta ya Elimu na Ajira,haya ndiyo ambayo Sheikh Ponda akiyasema nasi tutayasema daima.

Sasa kwa madai hayo ndipo Serikali hii ikaona eti Ponda ni mchochezi ndipo wakaona wampige risasi wakiamini kwamba watafunga midomo ya waislamu,tunaomba wajuwe wanajidanganya,hata Sheikh Ponda akifa lakini madai yetu bado yapo pale pale.

"Ikiwa Sheikh Ponda anapigwa risasi kwa madai ya wazi kabisa,mbona maaskofu wametoa waraka wa kumkashifu Rais Kikwete na hawajakamatwa wala kupigwa risasi,mbona kuna viongozi wa vyama vya siasa wamesema watahakikisha nchi haitaliki na wanafanya vurugu kila kukicha bila kukamatwa wala kupigwa risasi,naomba Serikali ifahamu kwamba amani pasipo kutenda haki ni sawa na kiini macho,na kwa kasi hii wanayotupeleka,wajuwe kwamba itafika hatua hali itakuwa mbaya kwetu sisi na kwao wao,kwani tutakaposema basi kuonewa kwetu itakuwa bora kufa kuliko kuishi".alisema

Naomba Serikali ifahamu kwamba kama wao wataona kwetu sisi waislamu kufa kwetu ni lazima kwa sababu ya kuzungumza bayana dhulma munazotufanyia,basi jiandaeni kutumaliza sote,lakin katu hatutonyamaza”,mwisho wa kumnukuu.

 
 SHEIKH KONDO WAZIRI AKIWASILISHA TAMKO LA WAISLAMU JIONI HII KATIKA VIWANJA VYA MWEMBE YANGA
 
HILI NDILO JERAHA LA RISASI KATIKA MWILI WA SHEIKH PONDA.

  
  TAKBIIR,WAISLAMU WAKISIKILIZA TAMKO WAKATI SHEIKH KONDO AKIWASILISHA TAMKO HILOJIONI HII.

kwaniaba ya bofya hapa

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA