Oct 11, 2013

Video: Kontena lenye vitu vya ajabu na vya kichawi lapatikana Kenya

Video: Kontena lenye vitu vya ajabu na vya kichawi lapatikana Kenya
Kontena lililokuwa na mzigo wa vitu vya ajabu limepatikana kwenye bandari ya Mombasa jana. Mzigo huo ulikuwa umefungwa kwenye katoni 10 kubwa zilizokuwa na mafuvu ya plastic ya binadamu, miguu, mikono, maiti (za plastic) na vitu vingine vya ajabu ajabu.
Afisa wa mamlaka ya mapato ya Kenya alisema vitu hivyo viliagizwa kutoka China na mwanasiasa maarufu wa Kenya. Alisema mzigo huo haujaruhusiwa kutoka bado. Inasemekana vitu hivyo vinahusiana na mambo ya kishirikina.
Uchunguzi kuhusu mzigo huo umeanza kufanyika na yule aliyeuingiza nchini humo atatajwa. Miongoni mwa vitu hivyo ni pamoja na ile inayomuonesha mtu akihangaika na kulia kwa maumivu makali na anashambuliwa na panya. 



chanzo na times fc

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA