Young Africans ambayo iliwasili katika mji wa Bukoba majira ya saa 5 asubhi ikitokea jijini Dar es salaam ambapo ilipitia jijini Mwanza kabla ya kutua kwenye mji huu ambao una mandhari mazuri na hali ya hewa safi.
Kocha mkuu wa Yanga mholanzi Ernie Brandts ametumia muda wa masaa mawili kuwafua vijana wake 21 ili kuwa fit kuelekea mchezo huo wa jumamosi ambao ni muhimu kwa Yanga kupata pointi 3 ili kujiweka katika mazingira mazuri.
Timu ilipolekelea uwanja wa ndege na umati mkubwa wa wapenzi na washabiki wa Yanga ambao walisema wamefurahia kuiona timu yao tena ikiwa katika mji huu na kusema watashilikiana bega kwa bega kuhakikisha timu inapata pointi 3 kwenye mchezo huo.
Kesho jioni Young Africans itafanya mazoezi katika uwanja wa kaitaba yakiwa ni mazoezi ya mwisho kabla ya mchezo huo wa siku ya jumamosi.
Wachezaji waliofanya mazoezi leo jioni ni:
Walinda Mlango: Ally Mustapha 'Barthez', Deogratius Munishi 'Dida' na Yusuph Abdul
Walinzi : Mbuyu Twite, Juma Abdul, David Luhende, Oscar Joshua, Nadir Haroub 'Cannavaro', na Kelvin Yondani
Viungo: Haruna Niyonzima, Athuman Idd 'Chuji', Frank Domayo, Nizar Khalfani, Mrisho Ngassa na Saimon Msuva
Washambuliaji: Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza, Jerson Tegete, Hussein Javu, Said Bahanuzi na Abdallah Mguhi 'Messi'

0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA