Nov 19, 2013

Rage asimamishwa Simba


Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage amesimamishwa na kamati ya utendaji ya klabu hiyo iliyokutana jana baada ya kukiuka miiko ya uongozi na kukiuka katiba ya klabu hiyo.

Hatua hiyo inakuja siku moja baada ya Rage kuwasainisha mkataba wachezaji wawili kutoka Zanzibar Ally Badru na Awadh Juma aliyekuwa anacheza Mtibwa.


Mabosi wa Simba wamethibitisha kusimamishwa kwa Rage na wanatarajia kuliweka wazi mbele ya waandishi wa habari kwa kina.


Taarifa ya awali inadai kuwa Rage amekuwa hajishughulishi kwa karibu na timu hiyo lakini pia amekuwa akikiiuka baadhi ya mambo ndani ya katiba na ndio maana kamati ya utendaji imepata nguvu ya kumsimamisha kwenye kikao hicho cha jana. 


chanzo na http://supermariotz.blogspot.com

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA