Shabiki wa Arsenal amuua mtani wake wa Liverpool
Shabiki
wa Arsenal amuua mtani wake wa Liverpool nchini Kenya kutokana na
hasira....baada ya kichapo cha Jumamosi....Liverpool 5-1 Arsenal
Kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo wawili hao walianza malumbano baada ya mechi kati ya vilabu hivyo kumalizika hapo Jumamosi.
Wawili hao walikua katika baa moja iliyojaa mashabiki wa timu hizo mbili.
Shabiki wa Arsenal anayefanya kazi ya Boda Boda alijawa na hasira baada
ya timu yake kukemewa na shabiki wa Liverpool kiasi cha kumdunga
mwenzake kisu mara kadhaa, kabla ya kutoweka.
Watu waliokua karibu na eneo la tukio hilo walimsaidia mwathiriwa
aliyetambuliwa kama Anthony Muteithia na kumpeleka katika hospitali kuu
ya Meru ambapo alifariki dunia wakati akipokea matibabu.
Mkuu wa polisi eneo la Meru Tom Odero amesema wanamsaka shabiki huyo wa Arsenal ambaye amekwenda mafichoni.
Hapo Disemba mwaka jana shabiki wa klabu ya
Manchester United nchini Kenya kwa jina Jimmy Macharia alijiua baada ya
klabu hiyo kuendelea kuorodhesha matokeo mabaya.
Na mnamo mwaka 2012 Suleiman Alfonso Omondi
shabiki wa Arsenal alijitia kitanzi baada ya timu hiyo kushindwa kwenye
mechi. Ligi ya Premia nchini Uingereza huvutia ushabiki mkubwa nchini
Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla.
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA