MWILI WA ADAM PHILIP KUAMBIANA WATOLEWA MUHIMBILI, KULALA KWAKE BUNJU LEO
Mwili
wa Marehemu Adam Kuambiana ukiwa ndani ya gari la kubebea maiti baada
ya kuchukuliwa moshwari Muhimbili, unapelekwa nyumbani kwake, Bunju, Dar
ambako utalala huko kabla ya kuagwa Viwanja vya Leaders na kuzikwa
Kinondoni, kesho.
Waombolezaji wakiwa wamelifungua gari la kubebea maiti ili kuweka jeneza lenye mwili wa Adamu Kuambiana leo mchana.
Waombolezaji
wakilia kwa uchungu, mmoja akiwa amedondoka baada ya mwili wa Kuambiana
kuwekwa kwenye gari la kubebea maiti nje ya moshwari Muhimbili Dar.
Msanii wa Filamu Bongo, Dude akihojiwa na Global TV On Line nje ya moshwari, Muhimbili.
Mmoja wa wasanii wa Bongo Muvi akihojiwa na Global TV on line.
Dude(kulia),
Johari, (katikati) na msanii mwingine wakiwa nje ya mochwari, Muhimbili
wakisubiri mwili wa marehemu Adam Kuambiana kutolewa na kusafirishwa
kwenda Bunju, Dar leo mchana.
(PICHA NA DENIS MTIMA NA GABRIEL NG'OSHA/ GPL.)
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA