Apr 24, 2012

DIWANI AJITOSA KUSAIDIA UKARABATI UWANJA WA BONDE FC

Hatimae diwani wa Makumbusho mh Ally Haroub amejitosa katika kusaidia ukarabati wa uwanja wa Bonde Fc.diwani alifikia hatua hiyo baada ya kutembelea uwanja na kuona jinsi ulivyoharibika.

  Alipoalikwa katika kikao cha  wanakamati ya kukarabati uwanja alifika na ndipo alipowahaidi kuwa atashuhurukia uwanja kwani suala hilo lipo ndani ya uwezo wake na kwa kushirikiana na kamati ya uwanja anahuhakika wa kuifanya kazi hiyo bila tatizo.
 
 Pia katika kikao hicho kamati ndogo ya kusimamia ukarabati iliundwa na diwani akiwa mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo  akiwataja wajumbe wa katimati hiyo mratibu wa uwanja wa Bonde Fc ndugu  Rashid Maulid Banda alisema kamati inaundwa na watu watano  
 
Nae mwenyekiti wa kamati ya muda iliyoundwa ndugu Omary Maloki amehaidi atahakikisha kamati yake inafanya kila linalowezekana ili kufanikisha matengenezo ya uwanja kwa kuwatafuta wafadhili mbali mbali ili kufikia malego.
  1.    MWENYEKITI               OMARY     MALOKI
  2.    KATIBU                        RAMADHANI  FARAHANI
  3.    MJUMBE                       EMANUEL I ISHENGOMA 
  4.    NJUMBE                       MASOUD      HEMED
  5.    MJUMBE                       MH:  ALLY    HAROUB 
  6.    MJUMBE                       RASHIDI       BANDA   
 
Kutokana na hualibifu huo umesababisha timu kuwa na wakati mgumu kutokana wa kukosa uwanja wa kufanyia mazoezi hali iliyopelekea timu kuomba uwanja katika shule ya msingi Tuliani Magomeni jambo ambalo ni hatari kwa wachezaji wa under 14 kwani inawaladhimu kuvuka barabara.
Na hata eneo lenyewe linalotumika kwa mazoezi ni dogo hivyo kusababisha timu kukosa muda wa kucheza full game  kwani kila siku wanacheza open space hali ambayo imekuwa ikiwafanya vijana kupata sana tabu katika mechi kutokana na kuzoea kucheza katika stahili hii.
Pia hali hii imepelekea wachezaji wengi kukimbia na kwenda kufanya mazoezi katika viwanja vingine na wengine kufanya mazoezi siku mojamoja.
 
habari na mtandao wa bonde fc www.bondefootballclub.blogspot.com 

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA