Jul 25, 2012

AZAM FC YAITOA NISHAI SIMBA

Jana timu ya Azam ilizidi kuonesha ubora wake katika michuano ya Kagame baada ya kuifunga timu ya Simba jumla ya goli 3-1 

Magoli yote ya Azam fc yalitupiwa kimiani na mshambuliaji hatari wa timu hiyo John Bocco goli la kwanza ilikuwa dk 16, 46, 76,

Goli la kufutia machozi la Simba lilifungwa na Shomari Kapombe dk 64  kwa matokeo hayo timu ya Simba itakuwa imeaga michuano hiii.

Kwa matokeo haya sasa Azam fc itkutana na Vita Club ya Congo katika mchuano wa nusu fainali 

Michuano hiyo itaendelea tena kesho kwa mechi mbili za nusu fainali 

Mechi ya kwanza ni kati ya Azam fc vs Vita Club saa 8 mchana, na mechi ya pili itakuwa kati ya bingwa mtetezi Yanga dhidi ya APR mechi zote zitachezwa katika uwanja wa taifa

    Hawa ni baadhi ya mashabiki wa simba waliofika taifa hapo jana

      hawa ni mashabikiwa wa Azam Fc wakishangilia timu yao

      Wachezaji wa Azam wakishingila moja ya magoli hapo jana 
      Kikosi cha Azam fc kilichoifunga Simba jana

Kikosi cha Simba kilichofungwa na Azam jana 

picha kwa hisani ya BIN ZUBEIRY

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA