Jana timu ya Azam ilizidi kuonesha ubora wake katika michuano ya Kagame baada ya kuifunga timu ya Simba jumla ya goli 3-1
Magoli yote ya Azam fc yalitupiwa kimiani na mshambuliaji hatari wa timu hiyo John Bocco goli la kwanza ilikuwa dk 16, 46, 76,
Goli la kufutia machozi la Simba lilifungwa na Shomari Kapombe dk 64 kwa matokeo hayo timu ya Simba itakuwa imeaga michuano hiii.
Kwa matokeo haya sasa Azam fc itkutana na Vita Club ya Congo katika mchuano wa nusu fainali
Mechi ya kwanza ni kati ya Azam fc vs Vita Club saa 8 mchana, na mechi ya pili itakuwa kati ya bingwa mtetezi Yanga dhidi ya APR mechi zote zitachezwa katika uwanja wa taifa





Kikosi cha Simba kilichofungwa na Azam jana
picha kwa hisani ya BIN ZUBEIRY
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA