Jul 4, 2012

Yanga yaanza kwa kupoteza


Kikosi cha pili cha mabingwa wa Kombe la Afrika Mashariki na Kati, Dar Young Africans kinachojiandaa na michuano ya Rollingstone kimekubali kufungwa goli 3-2 na Jamhuri ya Pemba, katika mchezo wa kombe la urafiki uliokwisha hivi punde.

Katika mchezo huo Yanga walikuwa wa mwanza kupata goli katika dakika ya 18 mfungaji akiwa Shaban Hamisi.

Jamhuri walifanikiwa kusawazisha goli hilo katika dakika ya 34, na kuongeza jingine katika dakika ya 45. Hivyo kupelekea Yanga kwenda mapumzika wakiwa nyuma kwa goli 2-1.

Katika dakika ya 69 Jamhuri walifanikiwa kuandika goli la tatu huku Yanga wakifunga goli lao la pili katika dakika ya 77 kupitia kwa Notekelly Masasi, na kupelekea mpira kumalizika kwa Yanga kufungwa goli 3-2.

Habari kwa niaba ya  http://aboodmsuni.blogspot.com/ wa   SPORTS IN BONGO

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA