Apr 23, 2013

Kim Poulsen atanga timu ya pili ya Taifa Stars


Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza timu ya pili ya Taifa (Young Taifa Stars) atakayoitumia kuangalia wachezaji ambao baadaye anaweza kuwajumuisha kwenye timu ya wakubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo (Aprili 23 mwaka huu) kabla ya kutaja kikosi hicho, Kim amesema timu hiyo ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliozinduliwa Aprili 4 mwaka huu ukilenga kuendeleza wachezaji.

Amesema timu hiyo inajumuisha wachezaji ambao wamepita umri wa kuchezea timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) na wakubwa ambao hawajapata fursa ya kuingia Taifa Stars, lakini atatumia Young Taifa Stars kuangalia uwezo wao.
“Timu hii ni kiungo kati ya vijana na wakubwa. Wengi wa wachezaji watakuwa vijana, lakini wakubwa wachache watapata fursa ya kuwemo ili kuangalia uwezo wao hata kama uko nyuma waliwahi kuchezea Taifa Stars. Lakini timu hii vilevile ni changamoto wa wachezaji wa Taifa Stars kuwa wapo wanaosubiri wazembee ili wachukue nafasi zao,” amesema.
Young Taifa Stars yenye wachezaji 30 itakuwa na kambi ya siku tano jijini Dar es Salaam kuanzia Mei 2 hadi 6 mwaka huu.
 -Chanzo TFF
Makipa
Aishi Manula Azam
Hussein Shariff Mtibwa Sugar
Ali Mustapha Yanga


Mabeki
Kessy Hassan Mtibwa Sugar
Kennan Ngoma Barnsley FC, Uingereza
Himid Mao Azam
Ismail Gambo Azam
David Mwantika Azam
Miraji Adam Simba
Mohamed Hussein Kagera Sugar
Waziri Salum Azam
Samih Nuhu Azam
Emily Mgeta Simba


Viungo
Haruna Chanongo Simba
Edward Christopher Simba
Mudathiri Yahya Azam
William Lucian Simba
Jonas Mkude Simba
Hassan Dilunga Ruvu Shooting
Jimmy Shoji JKT Ruvu
Abdallah Sesem Simba
Ramadhan Singano Simba
Farid Mussa Azam
Vicent Barnabas Mtibwa Sugar


Washambuliaji
Hussein Javu Mtibwa Sugar
Jerome Lambele Ashanti United
Zahoro Pazi JKT Ruvu
Twaha Hussein Coastal Union
Abdallah Karihe Azam
Juma Luizio Mtibwa Sugar

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA