Iran kujenga kituo kipya cha nyuklia
Dakta Fereydun Abbasi
Dakta Fereydun Abbasi Mkuu wa Shirika la Atomiki la Iran amesema kuwa,
Jamhuri ya Kiislamu ina mpango wa kujenga kituo kipya cha nyuklia.
Akizungumza na waandishi wa habari wa kigeni katika mji wa
Saint
Petersburg nchini Russia, Dakta Abbasi ameongeza kuwa, eneo la kujengwa
kituo hicho kipya limeshatengwa, na hivi karibuni Wakala wa Kimataifa wa
Nishati ya Nyuklia IAEA utajulishwa juu ya mpango huo. Abbasi ambaye
anahudhuria maonyesho ya kimataifa ya Atom - Expo 2013 na kikao cha
nishati ya umeme wa nyuklia katika karne ya 21 mjini Saint Petersburg
ameongeza kuwa, mikakati ya Iran ilikuwa ni kujenga tanuri la nyuklia
lenye uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 1,000 hadi 1,200 huko
Bushehr, ambapo moja kati ya miradi hiyo miwili tayari umeshaanza
kufanya kazi. Akizungumzia uwezekano wa kubadilishwa siasa za nyuklia za
Iran baada ya kuingia madarakani serikali ya Dakta Hassan Ruhani,
Mkuu
wa Shirika la Atomiki la Iran amesema kuwa, shughuli za nyuklia za Iran
zinafanyika kwa malengo ya amani kwa minajili ya kudhamini nishati ya
umeme na kuondoa mahitajio kwa wananchi na kwamba hakuna mabadiliko
yoyote ya kimsingi yatakayofanyika.
CHANZO NA http://kiswahili.irib.ir
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA