Jun 14, 2012

Taifa Stars Yajipanga Kuikabili Msumbiji





kikosi cha timu ya Taifa
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen amesema ili kuitoa Msumbiji ‘Mambas’ kwenye michuano ya Afrika ni lazima timu yake ishinde mechi ya marudiano itakayochezwa Juni 17 mwaka huu jijini Maputo.

Mechi ya marudiano kusaka tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 
zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa ulioko Zampeto nje kidogo ya Jiji la Maputo kuanzia saa 9 mchana kwa saa za huko.

Kim amewaambia Waandishi wa Habari leo (Juni 13 mwaka huu) kuwa maandalizi ya kikosi chake yanakwenda vizuri ingawa ana wachezaji watatu ambao ni majeruhi; kipa Mwadini Ali, na mabeki Nassoro Masoud Cholo na Waziri Salum.
Amesema wachezaji hao hawatakuwemo kwenye msafara wa timu hiyo utakaoondoka Juni 15 mwaka huu saa 11 alfajiri kwa ndege ya Kenya Airways kupitia Nairobi.

Kocha huyo amesema baada ya mechi tatu maendeleo kiuchezaji kwa timu yake inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ni mazuri ingawa bado anafanyia kazi kwa nguvu safu ya ushambuliaji. Mechi iliyopita Taifa Stars iliifunga Gambia 2-1 huku mabao yote yakifungwa na mabeki.

Iwapo Taifa Stars itaitoa Msumbiji katika raundi ya mwisho itapangiwa moja kati ya timu 16 zilizocheza Fainali za AFCON zilizofanyika Januari mwaka huu katika nchi za Gabon na Equatorial Guinea. Katika mechi ya kwanza dhidi ya Msumbiji iliyochezwa Dar es Salaam, Februari 29 mwaka huu timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.

Taifa Stars ambayo msafara wake utakuwa na wachezaji 20 itaagwa kesho (Juni 14 mwaka huu) saa 6 mchana kambini kwao- hoteli ya Accommondia (Tansoma) jijini Dar es Salaam.  Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kwa ajili ya kujenga afya kupitia mpira wa miguu.

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA