BREAKING NEWSSS:NAIBU WAZIRI TAMISEMI ATANGAZA MAJINA YA WANAFUNZI WATAKAOJIUNGA NA KIDATO CHA TANO
Nafasi za kujiunga na kidato cha tano mwaka 2014 kwa wanafunzi
waliomaliza mwaka jana zimetangazwa rasmi muda huu jijini dar es salaam
na naibu waziri wa TAMISEMI Bw KHASIM MAJALIWA ambapo zaidi ya
wanafunzi 16800 wamekosa nafasi hizo kutokana na sababu mbalimbali
ikiwemo upungufu wa shule za kidato cha tano.Akitangaza
majina na shule walizopangiwa wanafunzi hao Mh MAJALIWA amesema kuwa
jumla ya wanafunzi 54085 sawa na alisimia 75.61 ya wanafunzi 71527
waliostahili kuingia kidato cha tano mwaka huu wamechaguliwa huku
wavulana ni 31352 wakati wasichana ni 22733 ambapo ni sawa na ongezeko
la wanafunzi 20402 kwa kulinganisha na wanafunzi 33683 walochaguliwa
mwaka jana.
Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule
mbalimbali wataanza kuripot katika meneo yao tarehe 10 julai mwaka huu
ambapo mwisho wa kufika katika shule walizopangiwa ni tarehe 30 julai
mwaka huu ambapo amesema kuwa kwa wale ambao watakuwa hawajiripoti hadi
tarehe hiyo nafasi zao zitajazwa na waliokosa nafasi.
1.
Wasichana --- Shule Zote
<<BOFYA HAPA KUYASOMA MTANDAONI>>
AU
<< BOFYA HAPA KUYA DOWNLOAD>>
2.
Wavulana --- Majina ya Shule A Mpaka L
<<BOFYA HAPA KUYASOMA MTANDAONI>>
AU
<< BOFYA HAPA KUYA DOWNLOAD>>
3 .Wavulana --- Majina ya Shule M mpaka Z
<<BOFYA HAPA KUYASOMA MTANDAONI>>
AU
<< BOFYA HAPA KUYA DOWNLOAD>>
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA