Sep 1, 2014

BAADA YA KUTOKA HABARI KUWA ANATOKA NA DOGO DOGO LADY JAYDEE ATOA MAJIBU HAYA

  
Zamani ilikuwa haipo sehemu ya kujitetea, gazeti likishaandika ndio limeandika. 

Lakini sasa ulimwengu umebadilika, sio muda wa watu wote kulishwa chakula kisichofaa.

Kwanza hicho kichwa cha habari kimenivunjia heshma sana

Nafikiri lengo ni kuilazimisha jamii inayomuelewa JayDee tofauti imuone kuwa ni mtu asiefaa, sawa.

Dogo anaswa na mkoko? Huo mkoko mmemnasa nao wapi wakati hizo picha ni mimi nilizi post mwezi February Instagram?????

Picha ambazo zilipigwa Nyumbani lounge tena kutumia simu ya Gardner.

Jide, dogodogo gumzo mjini ๐Ÿ™†๐Ÿ™†๐Ÿ™†๐Ÿ™†
Gumzo ni kitu kinachoongelewa sana na kilichoenea kila kona ,,,,,sasa hii habari ni gumzo wapi ambapo haisikiki, ......


Mngeandika tumeamua kumuanzishia Jide gumzo hili, ndio ningewaelewa.
Vitu vya kuzua.


Ni watu wengi tu wakija band wakipata nafasi wanaomba kupiga picha na mimi na wengine pia wanaomba kupiga picha na gari sababu wanaipenda.

Kama mtu yoyote anavyoweza kupiga picha na sanamu la kitu chochote anachokipenda.

Hivi je! Wimbo wa JayDee mgumba, JayDee tasa umechuja? Umeisha chati?? Nashangaa na najiuliza tu
Inawezekana wimbo huo umechuja ndio maana mnatafuta wimbo mwingine utakao hit zaidi ya ule
Ndio kinachopelekea kuandika story za namna hii ๐Ÿ™‰๐Ÿ™‰๐Ÿ™‰๐Ÿ™‰๐Ÿ™‰๐Ÿ™‰๐Ÿ™‰๐Ÿ™‰


Sio nyinyi mliokuja kuomba radhi kwa yote mliowahi kuniandika na kudai kuwa mmejirekebisha, miezi kadhaa tu iliopita?

Sio boss wenu aliemfuata Gardner na kumwambia tumalize tofauti zetu?
Kama hizo tofauti zilikuwepo ๐Ÿ˜Ž๐Ÿ˜Ž๐Ÿ˜Ž


Inawezekana nyie ndio mna tofauti na mimi, sijawahi kuwa na tofauti na mtu hata nisiemfahamu. ..

Nashukuru Mungu nilikataa msamaha wenu ni kama nilihisi hamkumaanisha
Au sababu sijawahi kukubali show mlizotaka kufanya na mimi?

Je! Hiki ni kisasi? Sielewi
Mungu alienisimamia ataendelea
Hii sio vita ya kwanza wala ya mwisho
Dunia ni mapambano.


Kama nia ni kufanya niishi maisha ya uoga, kudhoofika na msongo wa mawazo mmefeli ,,,,, wengine mkijidai ni wacha Mungu huku mkiumiza nafsi za watoto wa binadamu wenzenu.
No wonder mnaishi bila amani mbali na utajiri mlionao kwa kuogopa visasi.

Sikuzaliwa kukata tamaa

Pia wapo wanaopenda kuandikwa kwenye hayo magazeti yenu
Wafanyieni favor ya kuwapa hiyo nafasi mi sifanyi muziki wa magazeti ya udaku
Mkiachana na mimi nitashukuru sana 


Hata ndoa yangu ikivunjika haimaanishi mnitafutie story za kunichafua
Ndoa ya Madiba ilivunjika sembuse yangu nina utofauti ipi na binadamu wengine?
Nyie ndoa zenu ziko perfect si ndio?


Hewala watakatifu nyie, mnaoficha yenu na kutangaza ya wenzenu.

Mwisho nawaomba watu mnaonielewa kutoamini tu habari yoyote ambayo haijatoka kwangu wala kwa muwakilishi wangu ambae ni "Webiro Wakazi Wasira".

Kama kuna chochote cha watu kujua nitakiongea mimi kwa mdomo wangu sio kuwekewa maneno mdomoni. 


Kila siku ooooh tulimpigia simu hapatikani, namba yangu yenyewe kwanza hata mnaijua???
Mngekuwa mnaijua msingekuwa mnahangaika mnawapigia watu wangu wa karibu kunitafuta , na hao watu hawawezi kunisaliti ndio sababu mpaka miaka 70 mtaishia kusema tulimpigia simu JayDee hapatikani.
Nyie muongee chochote mnachojiskia
Ila sie hatuna haki kujitetea ??

Hili nalo litapita kama mengine
Na inshallah nitakuwa hapa hapa nimesimama nawaangalia

Picha moja wapo ni hiyo ambapo mtoto wa vitoto alikuja siku hiyo hiyo na akapiga picha na Gardner, mbele ya gari hiyo hiyo mnayodanganya watu kuwa mmemkuta nayo na mahala ni hapo hapo Nyumbani Lounge, ,,,,, na picha nyingine ni hizo nilizowahi kuzi post mimi mwenyewe mwezi february leo zinanihukumu endeleeni kudanganya jamii 

Na hizo ni chat alizoniandikia huyo mtoto wa vitoto ambae ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona na sijawahi kumuona tena. . Zaidi ya kuongea nae twitter ,,, sisemi kama mimi malaika lakini
Ukweli huwa hauchanganywi na uongo

Kwa hili mmenidhalilisha sana

Kama nia yenu jamii inione mwanamke nisiefaa na ninaependa dogodogo
Basi Mungu atawaonyesha ukuu wake

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA