Jul 18, 2012

YANGA YAICHAPA WAU SALAAM 7-1-



Kikosi cha Young Africans Sports Club kilichoanza leo dhidi ya Waw Salaam




















Mabingwa watetezi wa kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (KAGAME) timu ya Young Africans Sports Club imeichapa bila huruma timu ya Wau Salaam ya Sudan mabao 7- 1 katika mchezo wa kundi wa C uliofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Young Africans ilianza mchezo kwa kasisi na kucheza pasi za kuonana, kwa dakika kumi 10 za kwanza huku ikifanya mashabulizi ya kushitukiza na katika dakika ya 12 mshambuliaji Said Bahanunzi aliipatia Young 

Africans bao la kwanza kwa kichwa kufuatia kumalizia kazi nzuri iliyofanywa na kiungo Haruna Niyonzima.
Dakika ya 17 ya mchezo mshambuliaji  Said Bahanunzi aliipatia Young Africans bao la pili, mara baada ya kumalizia kazi nzuri iliyofanywa na Hamis Kiiza na mfungaji kufunga bila ajizi akiwa ndani ya eneo la penati.

Huku ikicheza soka safi nala kuvutia, Young Africans iliendelea kulishambulia lango la Wau Salaam na dakika moja baadae dakika ya 18, Hamis Kiiza aliipatia Young Africans bao la tatu. 

Ikicheza mbele ya viongozi wake wapya na mwenyekiti mpya wa Young Africans Yusuf Manji , Hamis Kiiza Diego aliipatia Young Africans bao la nne dakika ya 25, na dakika tano baadae dakika ya 30 kiiza tena aliipatia Young Africans bao tano.

Hamis Kiiza aliendelea kuwa mwiba kwa wasudan hao, kwani katika ya 35 ya mchezo aliipatia tena Young Africans bao la sita  akimalizia krosi safi ya Haruna Niyonzima aliyeonekana kuisumbua Waw Salaam sehemu ya kiungo

Mpaka mpira unakwenda mapumziko, Young Africans ilikuwa mbele kwa mabao 6- 0.
Kipindi cha pilik kilianza kwa Young Africans kufanya mabadiliko ambapo ilimpumzisha Kelvin Yondani na nafasi yake kuchukuliwa na Juma Seif Kijiko, Rashid Gumbo akachukua nafasi ya Haruna Niyonzima, na Idrisa Rashid alichukua nafasi ya Stephano Mwasika.

Mabadiliko hayo yaliipa uhai timu ya Wau Salaam kwani ilianza kulishambulia lango la Young Africans na kutawala kidogo eneo la kiungo, huku washambuliaji wa Young Africans Kiiza, Bahanunzi na Nizar Khalfan wakikosa mabao ya wazi kutokana na kutokua makini.

Nizar Khalfan aliipatia Young Africans bao la saba katika dakika ya 75 kufuati kumalizia krosi safi iliyopigwa na Idrisa Rashid.

Huku watazamaji wakianza kutoka uwanjani wakijua Young Africans imeshinda mbao 7-0, Wau Salaam wailipata bao la kufutia machozidakika ya 92 ya mchezo, kufuatia kutokua makini kwa walinzi wa Young Africans.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika Young Africans iliibuka na ushindi wa mabao 7-1 dhidi ya Wau Salaam ya Sudan.

Young Africans iliwakilishwa na:
1.Berko, 2.Taita, 3.Oscar, 4.Cannavaro, 5.Yondan/Kijiko, 6.Chuji, 7.Nizar, 8.Niyonzima, 9.Bahanunzi, 10.Kiiza, 11.Mwasika/Idrisa

Young Africans itacheza tena mchwezo wake wa mwisho siku ya ijumaa dhifi ya vinara wa kundi C timu ya APR

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA