Jun 3, 2013

Azam FC haiachi walio na mikataba na haiongezi mchezaji mpya


Kama ilivyokuwa wakati wa dirisha kubwa la usajili 2012/13 ambapo Azam FC ilimuongeza George Odhiambo Blackberry pekee, safari hii tena Azam FC imeamua kwapandisha wachezaji wawili wa Under 20, Mudathir Yahaya na golikipa Hamadi Juma Yahya Kadedi na kufunga zoezi la usajili.

Kwa mujibu wa ripoti toka kwa Kocha mkuu wa Azam FC mtaalam Stewart Hall, hakuna sababu ya klabu kwenda nje kusajili wachezaji ambao viwango vyao havipishani na waliopo klabuni.

Mchezaji Abdulhalim Humoud amepata timu nchini Afrika ya Kusini, Abdi Kassim Sadala Babi mkataba wake umekwisha kama ilivyo kwa Deogratius Munishi Dida huku Uhuru Selemani akirejeshwa Simba SC baada ya kumaliza msimu wa mkopo na Azam FC.

Wachezaji wengine wote waliosalia wanabaki klabuni na kocha mkuu amependekeza baadhi ya makinda wa Under 20 walioonesha viwango vya juu wapandishwe timu kubwa, wapewe mikataba na kisha wapelekwe kwa mkopo ili wakapate nafasi ya kucheza. Wachezaji hao ni Omary Mtaki na Kevin Friday.

Azam FC ambayo imemaliza ligi ikishika nafasi ya pili kwa msimu wa pili mfululizo itaanza kambi ya kujiandaa na msimu mpya hapo June 24 kwa mujibu wa ratiba ya mwalimu na baada ya kumaliza kipindi cha pre season, kikosi cha Azam FC kitasafiri nje ya nchi kucheza mechi za majaribio kama ilivyo kawaida yake.

Wachezaji wanaounda kikosi cha Azam FC ni

Magolikipa; Mwadili Ally, Aishi Salum na Hamad Juma Yahya

Mabeki; Himid Mao, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Samih Nuhu, Luckson Kakolaki, Aggrey Morris, Said Moradi, David Mwantika na Jockins Atudo

Viungo; Kipre Bolou, Salum Abubakar, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo, Humphrey Mieno na Mudathir Yahya

Washabuliaji; John Bocco, Gaudence Mwaikimba, Khamis Mcha, Kipre Tchetche, Brian Umony na Abdallah Seif Karihe

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA