Jul 27, 2013

AZAM TV KUONYESHA LIGI YA VODACOM LIVE

 

Azam TV imefanikiwa kupata haki ya kuonyesha michezo ya ligi kuu Tanzania Bara moja kwa moja (live) inayo tazamiwa kuanza agosti 24 mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa toka global publisher Azam TV itaonyesha michezo isiopungua 60 Moja kwa moja (live) huku michezo 180 ikirushwa baada ya kurikodiwa.
Taarifa hizo zinaeleza kuwa Azam TV inayomilikiwa na kampuni ya Said Salim Bakharesa wamiliki wa Azam FC inayoshiriki ligi kuu ya Tanzania Bara, wameweka mezani kiasi cha Tsh bilioni 6.5 kwa shirikisho la soka Tanzania (TFF) kwa ajili ya kupata haki hiyo ya Matangazo.

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA