Jul 2, 2013

YANGA YAANZA MAZOEZI




















 Wachezaji wa Young Africans wakiwa mazoezini leo asubuhi

Kiungo mshambuliaji wa timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) Mrisho Khalfani Ngassa ni miongoni mwa wachezaji walioanza mazoezi leo asubuhi katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom 2013/2014 na mashindano ya kimataifa.

Yanga ambayo ilikuwa na mapumziko ya zaidi ya wiki mbili tangu kuahirisha kushiriki mashindano ya Kagame kufuatia serikali kuzizuia timu za tanzania kwenda kushiriki mashindano hayo kufuatia kuwepo kwa hofu juu ya hali ya usalama katika mji wa Darfur nchini Sudan.

Kocha Mkuu Ernie Brandts aliyekuwa mapumzikoni nchini Uholanzi alirejea jana na leo asubuhi ameongoza mazoezi ya asubuhi akishirikiana na kocha msaidizi Fred Felix Minziro ambapo mazoezi yalikuwa mazuri na kuvutia kwa wachezaji wageni.

Wachezaji waliofanya mazoezi leo ni pamoja na kiungo mshambuliaji Mrisho Ngasa aliesajiliwa msimu huu kama mchezaji huru akitokea tim ya Simba alipokuwa kwa mkopo akitokea timu ya Azam FC.

Mshambuliaji Shaban Kondo aliyejiunga na Yanga kama mchezaji huru akitokea nchini Msumbiji amefanya mazoezi pamoja na wachezaji wengine wote wa klabu ya Yanga ambao wataitumikia kwa ajili ya msimu mpya wa 2013/2014.

Kesho Yanga itaendelea na mazoezi asubuhi katika uwanja wa Loyola ambapo golikipa mpya alisejasiliwa kutokea klabu ya Azam Deogratius Munishi 'Dida' ataungana na wachezaji wengine katika mazoezi hayo ya kujiandaa na msimu mpya wa 2013/2014.

Wachezaji waliofanya mazoezi leo ni:
Ally Mustapha 'Barthez', Juma Abdul, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, David Luhende, Nadir Haroub 'Cannavaro', Salum Telela, Didier Kavumbagu, Jerson Tegete, Abdallah Mnguli, Nizar Khalfani, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Shaban Kondo.

Yanga itaendelea na mazoezi na siku ya ijumaa itasafiri kuelekea kanda ya ziwa kwa ajil ya kulitembeza kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na kucheza michezo kadhaa ya kirafiki.

NB: Yanga haijatangaza usajili wake wa wachezaji wa msimu mpya wa 2013/2014. 

 

















Mrisho Ngasa (katikati) akiwa mazoezini leo asubuhi katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola

CHANZO NA  http://youngafricans.co.tz 

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA