Kitendo hicho kilipokelewa kwa hisia tofauti na Serikali ya Kenya kwa kudai kwamba hatua hiyo iliyochukuliwa na Marekani sio sahihi.
Baada ya magaidi kuvamia kituo cha biashara cha Westgate nchini 
Kenya wiki iliyopita  ,Marekani imetoa onyo kwa raia wake kuacha 
kusafiri kuelekea nchini humo.
                
              
Kitendo hicho kilipokelewa kwa hisia tofauti na 
Serikali ya Kenya kwa kudai kwamba hatua hiyo iliyochukuliwa na 
Marekani  sio sahihi.
                
              
Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Wizara ya 
Mambo ya Nje ya Kenya ililaani vikali hatua ya Marekani ya kuwaonya raia
 wake kufanya safari nchini Kenya.
                
              
Taarifa hiyo iliitaja hatua hiyo kuwa, haina umuhimu na pia ilitolewa katika wakati ambao sio mwafaka.
                
              
Ripoti hiyo iliongeza kuwa, shambulizi la Westgate
 jijini Nairobi, ni tatizo la ulimwengu mzima hasa kwa kuzingatia kuwa, 
hata Marekani yenyewe imekwishaathiriwa na vitendo kama hivyo vya 
kigaidi.
chanzo na mwananchi.co.tz
  Dar Es Salaam Time
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA