Sep 25, 2013

YANGA YAJIANDAA KUIKABILI RUVU SHOOTING


KIKOSI CHA YANGA 

Young Africans imeendelea na mazoezi leo katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola-Mabibo kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom siku ya jumaosi dhidi ya maafande wa Ruvu Shooting katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Mchezo wa jumamosi ni muhimu kwa timu ya Young Africans kupata ushindi ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kutetea ubingwa wake na kupunguza tofauti ya pointi dhidi ya timu inayoongoza kwa tofauti ya pointi 5.

Kocha Mkuu wa Yanga mholanzi Ernie Brandts ameendelea kuyafanyia marekebisho makosa yaliyojitokeza katika michezo iliyopita kwa lengo la kuhakikisha vijana wake wanakua makini na kuzitumia vizuri nafasi wanazozipata.

Ikiwa imecheza mitano ikishinda mchezo mmoja, sare michezo mitatu na kufungwa mchezo mmoja, Young Africans imefanikiwa kukusanya pointii 6 na kufunga mabao 10 na kufungwa mabao 7.

Kikosi kinatarajiwa kuingia kambini kesho katika hosteli za klabu kujiandaa na mchezo huo wa jumamosi dhidi ya maafande wa Ruvu Shooting.

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA