Jan 22, 2014

OKWI APIGWA STOP YANGA

 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesimamisha usajili wa Emmanuel Okwi katika timu ya Yanga wakati likisubiri ufafanuzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kutokana na kuwepo na kesi tatu zinazomhusu Okwi, moja ikiwa imefunguliwa na Simba kuidai Etoile du Sahel malipo baada ya kumuuza mchezaji huyo,kesi ya pili ikiwa ni ya Okwi aliyoishtaki timu hiyo kutokana na kutolipwa mshahara wakati kesi ya tatu ikiwa imefunguliwa na Etoile ikimshtaki Okwi kwa utoro. 

TFF imeusimamisha usajili huo wakati ikiwa imewasiliana na FIFA kutaka kujua iwapo mchezaji huyo anaweza kucheza Ligi nchini Tanzania wakati Etoile du Sahel ikiwa imefungua kesi katika shirikisho hilo la kimataifa ikidai Okwi bado ni mchezaji wake.

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA