Kiungo mbrazil Emerson De Oliviera Neves Roque (kushoto) akisaini
mkataba leo wa kuitumikia klabu ya Young Africans, kulia ni Afisa Habari
wa klabu Baraka Kizuguto
Kiungo Emerson De Oliveira Neves Roque leo amesaini mkataba wa mwaka
mmoja kuitumikia klabu ya Young Africans baada ya benchi la ufundi
kuridhika na uwezo wake,na mchezaji mwenyewe kufikia makubaliano hayo ya
kuwatumikia watoto wa Jangwani.
Baada ya kufanya mazoezi kwa siku nne mfululizo chini ya makocha
Marcio Maximo, Leonardo Neiva na makocha wazawa Salavatory Edward,
Shadrack Nsajigwa kwa pamoja wameridhiswa na uwezo wake na kuomba apewe
kandarasi la kuitumikia klabu ya Young Africans.
Emerson aliyekua
akichezea katika timu ya Bonsucesso iliyopo daraja la pili kwenye jimbo
la Rio de Janeiro anachukua nafasi ya mshambuliaji Geilson Santos "Jaja"
ambaye ameshindwa kureje nchini kutokana na matatizo ya kifamilia na
kuomba klabu ya Young Africans imuache.
Kocha wa Young Africans
Marcio Maximo amesema wamerizishwa na uwezo na kiungo mkabaji Emerson na
kusema ataisaidia timu katika michuano mbali mbali ya Ligi na
Kimataifa.
Ujio wa Emerson unafanya klabu ya Young Africans
kufikisha jumla ya wachezaji watano wa kimataifa, wengine wakiwa ni
Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima, Hamis Kizza na Andrey Coutinho.
BONDE FC NI MABINGWA WAPYA WA BEIRA YOUTH CUP 2012
-
Timu ya Bonde fc jana iliibuka kuwa mabingwa wapya wa BEIRA YOUTH CUP 2012
ubingwa huo umepatikana baada ya kuibuka na ushindi wa gili 5-4 dhidi ya
New Bo...
11 years ago
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA