Mar 22, 2012

MAELFU WAJITOKEZA KUMSIKILIZA PROFESA LIPUMBA DAR JANA



Sehemu ya maelfu ya wananchi wakimsikiliza prof lipumba jana. Ameahidi CUF itasimamia ajenda ya kuhakikisha sehemu ya fedha zinazotokana na rasilimali pamoja na maliasili za nchi kama vile dhahabu na almasi zinagawiwa kwa wananchi wa Tanzania. Goo ni kwa sababu CCM wameshindwa kuinua maisha ya mtanzania huku serikali ikifuja fedha zinazotokana na rasilimali ambazo mungu amewapa watanzania wote. Prof lipumba amewaomba watanzania kuiunga mkono ajenda hii na kuhakikisha inakuwa sehemu ya mapendekezo ya katiba mpya ili chama chochote kikiingia madarakani suala la mgawanyo wa haki wa rasilimali za nchi usiwe mjadala. Goo Ni ajenda namba moja ya CUF kwenye mapendekezo ya katiba mpya na Ni ajenda kuu ya CUF Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, wale waliozoea sera za kukopi hapa wataula wa chuya. T 2015 CUF.


 Profesa Ibrahim Lipumba akihutumia maelfu ya wakazi wa Dar Es Salaam katika viwanja vya Mwembeyanga jana 21/03/2012 maelfu ya wafuasi wa CUF waliuzulia kumsikiliza mwenyekiti wa chama anasemaje kuhusu mwenendo wa chama kwa sasa

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA