Jul 26, 2012

NUSU FAINALI YA KAGAME NI LEO

Mashindano ya Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati almaarufu Kombe la Kagame 2012, yamefikia hatua ya Nusu Fainali ambapo timu nne(4) zitachuana siku ya alhamis kusaka timu timu mbili ambazo zitacheza fainali siku ya jumamosi katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.


Mabingwa watetezi wa kombe hilo klabu ya Young Africans itashuka dimbani kucheza na tim ya APR kutoka Rwanda katika nusu fainali ya pili itakayofanyika jioni majira ya saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Nusu Fainali ya kwanza itaanza majira ya saa 8:00 mchana kwa kuzikutanisha timu za Azam FC (Tanzania) na timu ya AS Vita ya (DRC), timu ya Azam imefanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali baada ya kuitoa timu ya Simba SC ya Tanzania pia kwa jumla ya mabao 3-1.

AS Vita nayo imefanikiwa kufika hatua hiyo ya nusu fainali baada ya kuifunga timu ya Atletico FC ya nchini Burundi kwa mabao 2-1 katika mchezo uliochzwa hapo awali.

Young Africans iimefanikiwa kufika hatua ya nusu fainali baada ya kuitoa timu ya Mafunzo ya Zanzibar kwa mikwaju ya penati 5-3, kufuatia kumalizika kwa dakika 90, ztimu zote zikiwa sare ya mabao 1-1.
APR kutoka Rwanda iliifinga timu ya URA kutok Uganda mabao 2-0 katika mchezo wa robo fainali na hivyo kupata tiketi ya kucheza hatua ya nusu fainali.

Kocha mkuu wa Young Africans Tom Saintfiet akiongea na tovuti ya klabu wwww.youngafricans.co.tz alisema anajua mchezo dhidi ya APR ni mgumu, kwani mchezo wa kwanza tulishinda kwa mabao 2-0, hivyo naamini APR wataingia Uwanjani wakiwa na nia ya kusaka ushindi tu ili waweze kucheza hatua ya fainali.

Saintfiet pia alisema pamoja na kuwa na mchezo huo mgumu dhidi ya APR, anaamin vijana wake wako katika hali nzuri ya ushindi, na maandalizi yote ya mchezo yamekamilika, hivyo anaamini timu yake Young Africans itaibuka na ushindi katika mchezo huo.

                                                                                                                       kikosi cha yanga kilichoifnga mafunzo kwenye hatua ya robo fainali 

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA