YANGA, NJOROGE MAMBO SAFI
Kaimu Katibu Mkuu wa Young Africans Sports Club - Lawrence Mwalusako
Uongozi
wa klabu ya Young Africans umemalizana na mchezaji wake wa zamani John
Njoroge aliekua na madai yake ya kuvunjwa mkataba wake miaka miwili
iliyopita, hali iliyompelekea Njoroge kuishtaki Yanga FIFA na jana jioni
Uongozi umemalizana nae.
Akiongea na mtandao wa klabu www.youngafricans.co.tz
katibu mkuu wa Young Africans Lawrence Mwalusako amesema wamefikia
mwisho juu ya suala na hilo ambapo jana jioni Njorogen alipokea pesa
aliyokua akidai klabu ya Yanga.
Awali tulitangulia kumlipa tsh
milioni 4 ambapo alitaka kumaliziwa pesa yake kwa pamoja, na jana klabu
ya
Young Africans ilimalizia kumlipa tshs milioni 14 kama alivyoelekeza
na hivyo Yanga kuwa imemlipa jumla ya tshs milioni 17 alizokuwa anadai
alisema 'Mwalusako'
Mchezaji John Njoroge aliyejiunga na Young
Africans akitokea Tusker FC ya Kenya amelipwa jumla ya tshs milioni 17
ambazo tayari amedhibitisha kuzipokea na kutuma kiambatanisho cha malipo
FIFA
John Njoroge alisajiliwa Young Africans mwaka 2008 kwa
mkataba wa miaka miwili kabla ya kuongezewa tena mkataba wa mwingine
ambao ulilkua na utata hatua iliyopelekea Njoroge kwenda kuishitaki
Yanga FIFA.
Kufuatia hatua hii Uongozi wa Young Africans
unawashukuru wapenzi, washabiki na wanachama wake kwa kuwa na subira
katika kipindi hiki ambacho uongozi ulikuwa unalishulikia suala hili.
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA