Oct 29, 2013

Mtatiro: Operesheni ya kusaka wahamiaji haramu imejaa unyamaa

rooo


1. Mtangazaji nguli na mmiliki wa kituo cha redio FADECO ya Karagwe Ndugu. Sekiku amenyang’ anywa pasi yake ya kusafiriwa na kuwekwa katika kifungo cha ndani ya nyumba yake, haruhusiwi kutoka.( redio yake imekuwa na msimamo imara katika kutetea maslahi ya wananchi kuliko kuwabeba watawala- nadhani sasa analipiziwa kisasi)

2. Diwani wa CUF huko Tunduru amevamiwa na wanajeshi hao wakidai ana pembe za ndovu, wakasachi nyumba nzima bila kupata chochote kibaya, badala ya kumwachia wamempiga usiku kucha na kumshikilia kwenye kambi maalum siku 2, kisha ati ndo wamemfikisha mahakamani.

3. Kijana mmoja huko Ulanga ameuawa kinyama na askari hao, mwenzie amepigwa sana na melazwa St Francis Ifakara, huyu alopigwa eti kosa lake ni kumiliki nyumba ya kifahari na gari aina ya Noah, askari wamempiga akizimia mara tatu. Wanamlazimisha akiri ati amejenga nyumba yake kwa biashara za ujangili.

4. Katika wilaya za Kondoa, Kilwa na Kilindi, wananchi wanavamiwa na wanajeshi na askari wanyamapori na polisi, wanapigwa mno, wengi hawaelewi kwa nini oparesheni hii ya kinyama inafanyika.

Haya na mengi yanafanyika kuhu serikali ikiwa kimya kabisa, inaona ni matendo ya kawaida sana. Hakuna anayechukua hatua kutokomeza vitendo hivi. Haiwezekani miaka 50 baada ya uhuru majeshi ambayo yanalipwa kodi za masikini yanatumiwa kuwapiga, kuwatweza, kuwadhalilisha nakuwaumiza raia wasio na hatia.

Watanzania waliichagua serikali ya CCM wakitaka maendeleo, si kuvunjiwa haki na utu namna hii. Nchi yetu imepoteza kabisa misingi ya utu na haki. Kama viongozi walioko serikalini wamekaa kimya haya yakiendelea, raia wa kawaida wafanye nini?

Binafsi huwa naguswa sana na matukio ya uvunjwaji wa haki za binadamu. Nimewapigia wakuu wa mikoa kadhaa, wakuu wa polisi kadhaa na hata kuongea na baadhi ya mawaziri. Kila mmoja anajidai hajui tatizo hili au liko nje ya uwezo wake? Hivi taifa hili linakwenda mbele au linarudi nyuma?

Natoa wito kwa wananchi wote kusimama kidete na kutumia nguvu zote zinazohitajika kusimamisha unyama huu. Kama pana watu wanahisiwa ni majangili waplekwe mahakamani ili haki itendeke. Kwa nini wapigwe hadi kufa au kuachiwa ?
chanzo na http://cuftz.com/

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA