Jan 14, 2014

Abiria 48 wanusurika kufa baada ya basi la Shabiby kuanguka Singida.

Abiria arobaini na nane waliokuwa wakisafiri na basi la shabibu kutoka arusha kuelekea  Dodoma wamenusurika kufa huku 28 wakijeruhiwa baada ya basi lao kutaka kulipita lori la mafuta wakati basi lingine la Princes Munaa nalo likiwa linalipita basi la Shabibu  katika mlima Kisaki na kusababisha basi la Shabibu kuanguka.

Wakieleza kondakta wa basi hilo aina ya Yunton lenye usajili wa namba T 930 BUW ambaye amevunjika miguu yote miwili  bwana Thadei Muhando na mkaguzi wa basi la Shabubu bwana Williamu Ofyenge wamesema wakati basi lao lilikuwa liki lipita lori la mafuta gafla waliona basi lingine  liki wapita na kuwa magari matatu katika njia moja  na hatimaye dereva wao alishindwa kulimudu basi lao na kusababisha kupinduka.

Mganga mfawidhi wa  hospitali ya mkoa wa singida daktali banuba deogratius amethibitisha kupokea majeruhi  ishirini na nane ambao wanapatiwa matibabu na mgonjwa moja ambaye alikuwa kondakta wa basi amevunjika miguu yote miwili na wanampatia matibabu.

Kwa upande wake dereva wa roli la mafuta aina ya benzi lenye usajili wa namba raa 496n na tela lake lenye usajili wa namba rl 0255  ambalo lilikuwa likitokea nchi ya Rwanda bwana Hadimana Benjamini amesema alipitwa na mabasi mawili na moja  likamgonga upande wake na hatimaye kuanguka .

Mkuu wa wilaya ya Singida mwalimu Queen Mlozi ambaye alifika katika ajali hiyo pamoja na kuwatembelea majeruhi amewataka madereva wote kuzingatia sheria za barabarani  ilikuweza kunusuru uhai wa watu na majeruhi.

 
CHANZO NA ITV

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA