Jan 21, 2014

Exclusive interview na Professor Jay kuhusu Mwanalizombe Studios, D'Knob na Suma G ni wasanii wa mwanzo kufanya kazi (Audio)



Mchawi wa Rhymes, Mr. Red Carpet, Professor Jay ama Joseph Haule kwa jina la kuzaliwa amefungua rasmi studio yake binafsi inayojulikana kama ‘Mwanalizombe Studios.

Tovuti ya Times Fm imefanya interview exclusively na mkongwe huyo katika game la Bongo Flava mwenye heshima kubwa katika game.

Mwanzo kulikuwa na tetesi kwamba Duke ndiye ambaye angekuwa producer wa Mwanalizombe Studios, lakini Professor Jay amesema kuwa producer atakayefanya kazi katika studio hiyo anaitwa ‘Villy’, jina geni kwa wengi lakini anauwezo mkubwa.

Fuatilia interview yote hapa:

Je, studio ya Mwanalizombe imewasaini baadhi ya wasanii kuwa label, na kama bado kuna mpango huo?

Huu ni mwanzo bado na hatuwezi kuahidi vitu vingi sana, kwa sababu watu wa label ni lazima tuangalie talent na nini, na talent lazima tuzitafute, talent haziko Dar es Salaam pekee. Na ndio maana katika tangazo letu tulilolitoa tumeweka email na namba za simu kiasi kwamba tunaweza kuangalia talent hapa na pale. Lakini so far, hakuna mtu ambaye tumeshamsaini officially kwamba yuko Mwanalizombe.

Lakini nia na madhumuni ya kuanzisha Mwanalizombe ilikuwa ni kuangalia pia na talent, kwa sababu tumeona talent nyingi zimekuwa mchangani haziwezi kushine kwa sababu gharama za studio zimekuwa kubwa na vitu vingine kama hivyo, kwa hiyo tunaaangalia jinsi gani tutawaboost. Hatuwezi kusema kwamba tutawarekodi bure kwa sababu uwezo hatuna wa kufanya hivyo kwa sababu kuna umeme kuna kodi na kuna bili hatuwezi sema tutafanya free. Lakini tunataka kuangalia talents ambazo zipo zimejificha ili ziweze kuonekana.

Kwa sababu sasa hivi tunasikia kuna wasanii wengi wanasikika lakini wengi hawana zile talents ambazo mimi nazijua. Nimepita mikoa mingi nimeona kuna talent za hatari lakini bado hazijapata nafasi. Kwa hiyo bado ni mwanzo lakini nadhani huko mbele tutaweza kuwasaini watu na tutaweza kuwa nao kwa sababu tunataka tuupeleke muziki wetu kwenye next level.
Ni sapoti gani umepata kutoka kwa wadau wengine wa muziki kuiinua studio yako? 

Cha kwanza ilikuwa, watu wakisikia Mwanalizombe...nilikuwa nawaambia tu kwamba kuna studio nilikuwa naifanya, lakini pia nilikuwa napata tatizo la maproducer. Kuna maproducer ambao wamenisaidia kuifanya Mwanalizombe iwe hapo ilipo. Mtu kama Dunga alinisaidia tangu naanza kununua vyombo, vingine nilinunua hapa na vingine nilivinunua ng’ambo nilikuwa nikimpigia na yeye ananishauri kufanya hiki na kile. Naye alikuwa interested kufanya kazi lakini amebanwa wana kazi zao ambazo wanafanya.

Mwingine ni Duke ambaye alinisaidia kufanya setup, kufunga ile studio na kufanya kila kitu. Duke naye amebanwa kuna biashara zake anazifanya lakini pia bado anatusapoti tuko naye pale. So, nilikuwa napata tabu kumpata producer ambaye anaweza kuendana na vyombo vyetu vya kisasa ambaye anaweza kupiga aina zote za muziki. Hatutaki kufanya aina moja tu ya muziki sijui Bongo Flava tu, hapana. Tunataka anakuja mtu anafanya mchiriku anafanya, mtu anafanya gospel anafanya na vitu vingine kama hivyo. Kwa hiyo ilikuwa ngumu hata kumpata Villy kwa sababu na yeye alikuwa anaprogram zake sema bahati mbaya alikuwa ana studio yake hiyo wakamuibia.

So, nadhani atatufaa pale kwa sababu anapiga kila aina ya muziki, ni mtu ambaye yuko humble, ni mtu ambaye nadhani kila mtu ambaye atakuja Mwanalizombe ataridhika.

Je, kuna baadhi ya kazi ambazo tayari Mwanalizombe imezifanya na umefanya na wasanii gani?

Sasa hivi ndio tumeanza kufanya kazi na akina D’Knob wanaingiza pale, akina Suma G na watu wengi ambao wameanza kuja kufanya, ma- underground wengi. Sipendi kuwaongelea sana kwa sababu kazi bado hazijakamilika na watu bado wanaendelea lolote linawea kutokea sio. Kwa hiyo itakapofika time tutasema sasa hii ni ngoma ya kwanza kutoka Mwanalizombe na vitu kama hivyo.
Kwa sasa hivi ndio tumejipanga rasmi kuanza kutoa nyimbo kutoka Mwanalizombe.

Sababu zipi zilipelekea uanzishe studio yako binafsi, na je, unadhani kuna gap lipi kwa upande wa studio Tanzania ambalo Mwanalizombe italiziba?

Sababu kubwa ya kuanzisha Mwanalizombe pamoja na kwamba nataka nisaidie artists…kwa sababu najua katika wasanii ambao geti lao linagongwa, langu linaongoza. Kila mtu anakuwa na imani kwamba Professor Jay anaweza kunisaidia na wengi wanakuja kuniomba hela za kwenda kurekodi studio. So, ili niweze kupata solution ya vitu vingi kwa mpigo nimeona kwamba nitengeneze studio, na hata gharama zao ambazo zitakuwa ni ndogo au zitakuwaje…lakini at least studio itapunguza geti langu kuweza kuyumbayumba na kugongwa na vitu kama hivyo.

Hiyo ni sababu ya kwanza, lakini sababu ya pili…mimi mwenyewe ni mwanamuziki, napata tabu saa zingine na maproducer pia sometimes sipati kazi yangu kwa wakati na vitu vingine, kwa hiyo kazi zangu pia ntazifanya. Sisemi kazi zangu zote ntazifanya Mwanalizombe, hapana, lakini itanirahisishia. Kuna kazi nyingine zinatakiwa ziende quick na kuna kazi zingine zinatakiwa ziende katika wakati lakini zilikuwa zinanisumbua na vitu vingine kama hivyo.

Na Mwanalizombe tumeita Mwanalizombe Studios kwa maana kwamba hatutakuwa tunafanya audio tu peke yake. Tumeagiza vyombo au vifaa pia vya video na pia tunaweza kufanya photo-shoot na vitu vingi ambavyo leseni yetu inatuonesha hivyo. So, tunaweza tukafanya hivyo vitu kwa wakati wowote lakini tumeanza na audio production kwa kuwa ni wakati wake na ndio kitu ambacho kinahitajika sana kwa kipindi hiki.

Sitaki kusema kwamba nakuja kuleta ushindani ama nakuja kuwa number one, hapana. Nakuja kufanya kufanya muziki kwa ajili ya kufanya mapinduzi mazuri, kwa ajili ya kufanya revolution na kuwasaidia watu kwa mafanikio ya muziki wa kizazi kipya.  

Mwanalizombe Studios inapatikana wapi, na endapo mtu anataka kuwapata atumie njia gani?
Mwanalizombe Studio iko Msasani mwisho karibu na Capetown Fish Market, watu wakaribie tu, watu wenye talent zao. Na email ni mwanalizombestudios@yahoo.com na mwanalizombestudios@gmail.com. Na namba tunazozitumia studio ni 0757919192.

Usikose kusikiliza The Jump Off ya 100.5 Times Fm, leo kuanzia saa mbili kamili usiku hadi saa nne kamili usiku. Unaweza kusikiliza Online kupitia link hii popote pale duniani

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA