VIONGOZI WANAPAMBANA KUONGEZANA POSHO, WANANCHI WANATESEKA NA UMASIKINI.,'' MTATIRO''
Masuala ya ajabu na aibu kama haya ya kuongezana posho wakati
mamilioni ya watanzania wanakufa na njaa, maradhi, huduma mbovu na
kukataa tamaa, hayakubaliki.
Wananchi masikini lazima waamke na
kupinga kwa nguvu masuala haya. Kama ikitokea wananchi wakaandamana
kupinga jambo hili ntawaunga mkono kwa asilimia mia moja.
Binafsi nitatimiza wajibu wangu bila woga, nitalipinga jambo hili
hadharani ndani ya bunge, na nitakataa nyongeza ya posho. Nitafanya lile
niwezalo.
Mtume Muhammad(SAW) aliwahi kusema, ukiona mtu
anatenda maovu jaribu kuzuia, ukishindwa kemea na ukishindwa basi chukia
jambo hilo.
Nimeanza mchakato wa kuwasiliana na wabunge wote
wanaopinga ongezeko la posho, natambua watakuwa wachache lakini sauti
zetu zitasikika, hata kama wengi wataka posho watatushinda, ukweli kuwa
msimamo wetu utaiamsha jamii, hata kama tutachekwa, ukweli ni kuwa taifa
linahitaji viongozi wathubutu na ambao haataona aibu kusema this is
wrong hata kama watachekwa na kudhihakiwa.
Hivi sasa taifa letu
limefikia mahali pabaya mno. Deni la taifa ni trilioni 27, hali ya
uchumi ni mbovu, mishahara ya wafanyakazi ni kiduchu, watoto wanakufa
kwa utapiamlo, wanawake wanajifungulia sakafuni, watoto wadogo wanakaa
kwenye mavumbi ili wasome, maji safi na salama hakuna, barabara ni mbovu
hazipitiki, wakulima hawana pembejeo, wazee wenye umri mkubwa na watoto
hawana matibabu ya uhakika.
Pamoja na yote hayo, viongozi
wanakutana na kuanzisha mjadala wa kuongezana posho. Posho ya shs laki
tatu inatosha sana na nmesema inabakia. Mjadala wa kuongezana POSHO ni
upuuzi na ninaupinga ndani na nje ya nafsi yangu, nitaupinga kwa maneno
na vitendo.
Kuna wabunge wa chama kimoja cha upinzani walinifuata wakiwa kundi, wakaanza kunihoji na kunicheka, ati napigana vita ambayo Zitto Kabwe
alishindwa, nikasikitika sana. Hoja zao ni kwamba hizo posho hata
zikipingwa zitaliwa na CCM hivyo ni bora ziliwe na sisi. Mie nikawaambia
CHANGE STARTS FROM YOU AND ME! Na nikawaambia SHAME IN YOU AND YOUR
GRAVES!
Vyama vyetu vikianza kuiga tabia za CCM au kujaribu
kuziishi, vitapoteza uhalali wa kuwakomboa watanzania. Vyama vyetu
lazima viwe mstari wa mbele kupinga matumizi makubwa yasiyo muhimu.
Watu wachache wanaweza kufikiri hii ni vita ndogo. Nawaambia kuwa hii
ni vita ya MAMILIONI YA WANANCHI dhidi ya VIONGOZI WACHACHE WALAFI ambao
matumbo yao hayatosheki. Vita hii itakwisha kwa wananchi kuwaondoa
madarakani viongozi WAFIKIRI KULA, WALAFI na WABADHIRIFU.
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA