Timu ya Young Africans Sports Club kesho siku ya jumamosi, itashuka
 dimbani kucheza dhidi ya timu ya Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi 
kuu ya Vodacom Tanzania bara, mchezo utakaofanyika katika Uwanja wa 
Taifa jijini Dar es salaam.
Young Africans itaingia uwanjani kwa lengo la kusaka
 pointi 3 muhimu ambazo zitapelekea kusogea katika nafasi tatu za juu, 
na baadae kuweza kuwa katika nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu 
ya Vodacom 2012/2013.
Katika mchezo wa mwisho 
dhidi ysa Toto Africans jini Mwanza, Young Africans iliibuka na ushindi 
wa mabao 3-1, shukrani kwa mabao ya Mbuyu Twite, Didier Kavumbagu na 
Jeryson Tegete.
Kocha mkuu wa Young Africans 
Sports Club, mholanzi Ernie Brandts amesema vijana wake wote wako safi, 
wanaendelea na mazoezi hivyo ana imani mchezaji yoyote atakayepangwa 
atafanya vizuri katika mchezo huo.
Wachezaji 
Kelvin Yondani na Said Bahanunzi ambao walikua majeruhi wanaendelea 
vizuri na mazoezi, lakini kwa mujibu wa daktari wa timu Dr Suphian Juma 
amesema wachezaji hao hawataweza kucheza mchezo wa kesho, kwani bado 
hawajawa katika hali nzuri, ila wanaweza kuanza kucheza mchezo dhidi ya 
Polisi Morogoro siku ya jumatano. 
Viingilio vya mchezo ni:
VIP A 20,000/=
VIP B & C 15,000/=
Orange 8,000/=
Blue & Green 5,000/= 
habari kwa hisani ya mtando wa yanga sport club
habari kwa hisani ya mtando wa yanga sport club
 

 
 Dar Es Salaam Time
  Dar Es Salaam Time 
 
 
 
0 Weka maoni yako hapa:
Post a Comment
COMMENT HAPA