Oct 19, 2012

YANGA NA RUVU KUCHEZWA TAIFA


 Timu ya Young Africans Sports Club kesho siku ya jumamosi, itashuka dimbani kucheza dhidi ya timu ya Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara, mchezo utakaofanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.



Young Africans itaingia uwanjani kwa lengo la kusaka pointi 3 muhimu ambazo zitapelekea kusogea katika nafasi tatu za juu, na baadae kuweza kuwa katika nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom 2012/2013.

Katika mchezo wa mwisho dhidi ysa Toto Africans jini Mwanza, Young Africans iliibuka na ushindi wa mabao 3-1, shukrani kwa mabao ya Mbuyu Twite, Didier Kavumbagu na Jeryson Tegete.

Kocha mkuu wa Young Africans Sports Club, mholanzi Ernie Brandts amesema vijana wake wote wako safi, wanaendelea na mazoezi hivyo ana imani mchezaji yoyote atakayepangwa atafanya vizuri katika mchezo huo.

Wachezaji Kelvin Yondani na Said Bahanunzi ambao walikua majeruhi wanaendelea vizuri na mazoezi, lakini kwa mujibu wa daktari wa timu Dr Suphian Juma amesema wachezaji hao hawataweza kucheza mchezo wa kesho, kwani bado hawajawa katika hali nzuri, ila wanaweza kuanza kucheza mchezo dhidi ya Polisi Morogoro siku ya jumatano. 

Viingilio vya mchezo ni:

VIP A 20,000/=

VIP B & C 15,000/=

Orange 8,000/=

Blue & Green 5,000/= 

habari kwa hisani ya mtando wa yanga sport club

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA