Nov 6, 2013

LIPUMBA AKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU WA DENMARK NA KUJADILI UCHUMI

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAREHE 06/11/2013

PROF LIPUMBA AKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU WA DENMARK: WAJADILI MATATIZO YA UCHUMI
.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Prof.Ibrahim Lipumba akutana na Naibu waziri mkuu wa Dernmark Bi. Margrethe Vestager kujadili mambo mbalimbali ikiwemo uchumi katika kikao kilichofanyika katika mji wa Copenhagen nchini Denmark.

Katika mazungumzo hayo walijdaili matatizo ya uchumi yanayokabila nchi za Ulaya hasa ukanda wa Euro vinavyoathiri nchi za Afrika ikiwemo Tanzania na hatua za kuchukua.

Mambo mengine yaliyogubiga mzungumzo hayo ni pamoja na tatizo la ajira kwa vijana ulimwenguni, Misaada ya Maendeleo kwa nchi maskini na ujenzi wa uhusiano mzuri kati ya CUF na chama cha Radikale Venstre.

Bi. Margrethe Vestager ambaye ni kiongozi wa Chama cha Radikale Venstre pia ni Naibu Waziri Mkuu katika Seikali ya Mseto ya Denmark inayojumlisha vyama vitatu vya Social Democrats, Radicale Venstre na Socialist People Party.

Majadiliano hayo yalifanyika wakati wa ziara ya ujumbe wa CUF Denmark kwa mwaliko wa chama cha Radicale Venstre.Ujumbe wa CUF ulijumuisha viongozi mbalimbali wa chama pamoja na wanachama uliofanyika kuanzia terhe 26Oktoba 2013 mpaka 3 Novemba 2013.

Imetolewa na
Abdual Kambaya
Naibu Mkurugenzi wa Haki za binadamu ,sheria na Habari CUF

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA