Apr 25, 2014

KUMEKUCHA COASTAL UNION MESEMAJI WAO ABWAGA MANYANGA


  
MIMI Hafidh Athumani Kido, nikiwa na akili timamu natangaza kutojihusisha na shughuli zote za Coastal Union, hasa usemaji wa klabu.

Miongoni mwa sababu nyingi zilizonifanya kutangaza uamuzi huo ni sintofahamu iliyozuka ndani ya klabu yetu, kwa taaluma yangu ya uandishi wa habari lazima niwe na msimamo juu ya mambo yanayoendelea kwenye jamii.


Ili niendelee kufanya kazi na klabu hii kwa wakati huu wa misuguano, lazima niwe na upande; kwa maana upande unaounga mkono uongozi ama upande usiokuwa na Imani na uongozi. Lakini mimi nimeamua kutounga mkono upande wowote.


Kwa hivyo basi, ili niwe katika mstari sahihi nimeamua kukaa pembeni nifanye shughuli zangu za uanahabari kwa furaha na amani. 


Bado ni mwanachama halali wa Coastal Union Sports Club, namba yangu ya kadi ni 0013. Nitaendelea kutoa ushauri na kuishabikia klabu yangu ambayo nimekuwa nikimuona marehemu baba yangu na kaka zangu wakiishabikia tangu nikiwa mdogo.

HAFIDH KIDO
DAR ES SALAAM, TANZANIA
0713 593894

0 Weka maoni yako hapa:

Post a Comment

COMMENT HAPA